Benedict Liwenga- WHUSM
WADAU wa Habari wameisifu Serikali kwa kuundaa na kuwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Huduma za Jabari.
Wamesema
ni jambo ambalo lilikuwa limesubiriwa kwa muda mrefu tangu mchakato
ulipoanza miaka ya 80 na baadaye kuzimika halafu na kurudi tena miaka ya
hivi karibuni hususani mwaka juzi na mwaka jana 2015.
Akiongea
kupitia kituo kimoja cha cha Televisheni nchini jana, Mhariri Mtendaji
wa Gazeti la Jamhuri na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini,
Bw. Deodatus Balile amesema amefurahishwa sana na Muswaha huu kuwataka
wanahabari kujiendeleza kitaaluma jambo ambalo amesema ni muhimu katika
taaluma yoyote.
“Kwa
kweli kuhusu Mwandishi wa habari kusoma au kuwa na digrii, hili
naliunga mkono, inabidi waandishi wasome na kama hawataki kusoma basi
wajaribu ujinga”, alisema Balile.
Naye
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw.
Hassan Abbas amesema kuwa Muswada huu ni muhimu kwa wanahabari na
taaluma ya habari kwa ujumla kwani ni kwa mara ya kwanza katika Tanzania
uandishi wa habari unaenda kuwa taaluma.
“Nipende
kuwaasa wana taaluma wenzangu kuusoma Muswada huu na kutoa maoni badala
ya kulalamika kwani sisi ndiyo tunaoielewa zaidi taaluma ya habari,
hivyo maoni yetu ni muhimu”, alisema Abbas.
Abbas
aliongeza kuwa, Muswada huo utafanya uandishi wa habari kuwa taaluma
inayoheshimika na utaanzisha Baraza Huru la Habari na Bodi ya Ithibati
ya wanahabari, mambo ambayo yamekuwa yakipiganiwa na wanahabari. Hivyo
Muswada huu ni wa manufaa kwa wanahabari.
Akiongea
katika ziara maalum aliyofanya Mkurugenzi wa MAELEZO katika ofisi za
Majira, Mhariri Mtendaji wa Majira, Bwana Emmnanuel Mbuguni alisema
kwamba amefurahishwa na kipengele cha wanahahabari kusoma ili kuongeza
weledi katika kazi yao. Hivyo, amesema kwa jinsi hiyo anakubaliana na
Muswada huo na akaahidi kutoa maoni yake zaidi kupitia barua pepe ya
Bunge.
0 comments:
Post a Comment