Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
Baadhi
ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini (GCU) wamemesema Muswada
wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016 ni muhimu kwa taifa na
unalenga kuleta tija kwa taifa zima.
Muswada huo unalenga kuwanufaisha waandishi wa habari, wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na wananchi wa kawaida nchini.
Wakipongea
kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hii, Wakuu hao leo wa
wamesema muswada huo una manufaa na fursa nyingi kwa taifa na wananchi
tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali.
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Zawadi Msalla amesema kuwa sheria hiyo inatoa mwanya mkubwa kwa
tasnia ya habari nchini kuwa ni miongoni mwa taaluma inayoheshimika
kama kada nyingine kwa kuwa na chombo kitakachowasimamia wanahabari hao.
“Uanzishwaji
wa Baraza Huru la Habari ni moja ya takwa lililowekwa na Sera ya habari
na Utangazaji ya mwaka 2003 iliyoitaka Serikali kuanzisha chombo huru
kitakachosimamia masuala ya habari hivyo,muswada huu utakapokuwa sheria
utakuwa umetekeleza agizo la Serikali la kuanzisha chombo huru
kitakachosimamia masuala ya habari”, alisema Msalla.
Zawadi
ameongeza kuwa kuanzishwa kwa Sheria hiyo itasaidia kuleta uhuru wa
vyombo vya habari na wanahabari kufanya kazi yao ipasavyo kwani kwa sasa
mmiliki wa chombo cha habari asiporidhishwa na maamuzi ya kutopewa
leseni anakata rufaa kwa Waziri mwenye dhamana na asiporidhishwa na
maamuzi yaliyotolewa na Waziri huyo amepewa fursa ya kwenda mahakamani.
Kwa
upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa
Morogoro, Andrew Chimesela amepongeza juhudi za Serikali kwa kazi ya
kuandaa Muswada ambao utasaidia kuwa na Sheria itawanufaisha wadau wote
wa habari nchini.
Baada
ya kupitishwa Muswada na Bunge, kuidhinishwa na kusainiwa na Rais
hatimaye kuwa Sheria, Chimesela kuwa ziandaliwe kanuni ambazo zinaendana
na wakati huu wa sasa tofauti na ilivyokuwa wakati wa Sheria ya
Magazeti ya mwaka 1976.
Aidha,
amekubaliana na uamuzi wa kuundwa kwa Bodi ya Ithibati kwa sababu bodi
hiyo itakua na kazi ya kuangalia maslahi ya wanatasnia pamoja na
kudhibiti nidhamu na maadili ambayo yanapaswa kwenda sambamba na tasnia
habari ili iweze kuheshimika kama taaluma nyingine za Wanasheria,
wahasibu na sekta ya afya.
Naye
Mkuu wa Kitengo cha GCU kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti,
Englibert Kayombo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Mfuko wa Taifa
wa Bima ya Afya (NHIF), wameunga mkono uanzishwaji wa Bodi ya Ithibati
kwasababu itasaidia kutambua wanahabari wenye taaluma halali kwenye
sekta ya habari nchini.
“Binafsi
naunga mkono jitihada zinazofanywa na Wizara za kurasimisha tasnia hii
ya habari ili iwe na hadhi sawa na tasnia zingine, ni vyema kuratibu
kazi za waandishi wa habari ili waweze kutoa habari zenye kujenga taifa
letu imara lenye mfumo mzuri wa kazi za kihabari”, alisema Kayombo.
Baada
ya kuanzishwa na kufanya kazi Sheria hiyo, ni dhahiri itavifanya vyombo
vya habari nchini kuajiri watu wenye taaluma ya habari tofauti na hali
ilivyosasa na wananchi watarajie kupata habari za ukweli na uhakika.
0 comments:
Post a Comment