Home » » Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imekabidhi msaada kituo cha watoto yatima mkoani Dodoma

Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imekabidhi msaada kituo cha watoto yatima mkoani Dodoma

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Habari mdau pokea codes,
Mlezi wa kituo cha watoto cha Rahman Ophanage Centre  cha mjini Dodoma  Shekhe Mohamed Thabiti (kushoto) akipokea masaada wa vyakula kutoka kwa Meneja wa Tigo kanda ya kaskazini inayojumuisha mikoa ya Dodoma ,Singida na Manyara Aidan Komba (kulia)  jana kampuni hiyo iliandaa futari  kwa Watoto wa kituo hicho na  kukabidhi msaada wa vyakula ,mafuta na sabauni vyote vikiwa na  thamani zaidi ya milioni 1.5.


Meneja wa tigo kanda ya kaskazini inayojumuisha mikoa ya Dodoma ,Singida na Manyara Aidan Komba (kulia) akimkabidhi msaada mtoto Halima Bakari kwa niaba ya watoto wa kituo cha kulelea watoto cha Rahman Ophanage Centre  cha mjini Dodoma  jana usiku wakati kampuni hiyo ilipoandaa futari   kwa Watoto wa kituo hicho na  kukabidhi msaada wa vyakula ,mafuta na sabauni vyote vikiwa na  thamani zaidi ya milioni 1.5.



Meneja wa tigo kanda ya kaskazini inayojumuisha mikoa ya Dodoma ,Singida na Manyara Aidan Komba (kulia) akishiriki kugawa futari kwa Watoto wa kituo cha Rahman Ophanage Centre  cha mjini Dodoma  jana usiku wakati kampuni hiyo iliandaa futari  kwa Watoto wa kituo hicho na  kukabidhi msaada wa vyakula ,mafuta na sabauni vyote vikiwa na  thamani zaidi ya milioni 1.5.

Wafanyakazi wa kampuni ya simu ya mkononi ya Tigo wakishiriki futari ya  jioni na watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Rahman Ophanage Centre  cha mjini Dodoma jana usiku wakati kampuni hiyo iliandaa futari na kutoa msaada wa vyakula ,mafuta na sabauni vyote vikiwa na  thamani zaidi ya milioni 1.5.



Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imekabidhi msaada wa chakula na kuandaa futari kwa ajili ya  Watoto wanaishi kwenye kituo cha kulelea watoto cha Rahaman Ophanage center cha mjini Dodoma .

Msaada huo ulikabidhiwa jana kwenye kituo hicho  na timu ya Wafanyakazi wa kampuni ya simu ya Tigo Mkoa wa Dodoma  ikiongozwa na    Meneja wa Tigo kanda ya kaskazini  Aidan Komba .

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo meneja wa Tigo kanda ya kaskazini  inayojumisha mikoa ya Dodoma ,Singida  na manyara  Aidan Komba alisema kampuni ya tigo wameamua kutoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kushirikiana na jamii hasa wenye mazingira magumu.

Komba alisema msaada huo ni sehemu ya faida ambayo kampuni inarudisha kwenye jamii kwa kuwaunga mkono katika kununua na kutumia mtandao wao.

Alisema mwaka huu tigo walichagua kushiriki kuandaa futari na kutoa msaada wa vyakula kwa Watoto wanaotunzwa katika kituo hicho ili           wao waone kuwa Kampuni  inawajali  na  kushirikiana  nao .

Alitaja aina ya vitu    walivyokabidhi hapo jana katika kituo hicho kuwa ni  mchele ,unga wa ngano,unga wa chakula,mafuta ya kupikia na sabuni za kufulia na kuogea.
Aidha laisema vifaa hivyo walivyokabidhi thamani yake ni zaidi y ash milioni 1.5 na kuwa vyakula hivyo walivyokabidhi vitasaidia kuendelea kupata futari kwa siku za kufunga zilizobaki.

Naye mmoja wa Watoto wanaotunzwa katika kituo cha Rahaman Ophanage Center cha Chang'ombe mjini Dodoma ,  Halima Bakari aliwashukuru wafanyakazi wa  kampuni ya tigo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia msaada huo mkubwa.

Kwa upande wake mwalimu wa kituo hicho Ustadhi Umas Mafita  aliishukuru menejimenti ya kampuni ya Tigo kwa kutoa msaada na kuwapa futari watoto wa kituo hicho 
Alitoa wito kwa makapuni mengine kuiga mfano wa kampuni ya tigo  na kijitokokeza kukisaidia  kituo hicho chenye watoto zaidi ya 100 wanaotunzwa hapo  .

Alisema idadi hiyo ya watoto wanaotunzwa  pamoja na kupewa mafunzo ya kidini ya kislamu  na elimu ya kawaida .


Mafita aliwaomba tigo kuendelea kuwasaidia kituo hicho kwani kinamahitaji mengi kama vifaa vya shule,magodoro, vitanda na ujenzi wa mabweni .




0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa