Home » » WANYAMAPORI HAI WAMEKUWA KIFUTIO KIKUBWA KATIKA BANDA LA TAWA KWENYE MAONESHO YA NANE NANE, DODOMA

WANYAMAPORI HAI WAMEKUWA KIFUTIO KIKUBWA KATIKA BANDA LA TAWA KWENYE MAONESHO YA NANE NANE, DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Katika kuadhimisha maonesho hayo ya Nane Nane yanayofanyika viwanja vya Nzuguni nje kidogo ya mji wa Dodoma, banda la Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania- Tawa limekuwa kivutio kikubwa kwenye maonesho hayo ambayo yameanza rasmi tarehe 1/8/2017.

Kivutio hicho kimetokana na kuleta wanyamapori mbalimbali wakiwepo Simba, Chui, Nyati, Chatu, Nyoka mbalimbali, Ndege mbali mbali, Fisi na Tausi. Kwa mara ya kwanza maonesho haya ya kuleta wanyamapori hai yalikuwa yanafanywa na Idara ya Wanyamapori. Safari hii TAWA wameamua kuongeza idadi ya wanyama ambayo haikuwapo hapo awali. Mfano Nyati na Mamba.

Akizungumza katika maonesho hayo, Afisa habari na Mahusiano wa TAWA Bw. Twaha Twaibu aliwaeleza Wandishi wa Habari kuwa TAWA inashiriki kwa mara ya kwanza katika maonesho haya. Aliendelea kusema TAWA ni Mamlaka iliyoanzishwa kwa Amri ya Serikali na kutangazwa kwenye gazeti la Serikali Na.135 la tarehe 9 Mei, 2014. Uanzishwaji wa Mamlaka hii ni utekelezaji wa kifungu cha 8 cha Sheria ya kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009. Mamlaka ya Wanyamapori imeanza kazi rasmi tarehe 1/Julai/2016. Makao Makuu yake kwa sasa yapo mjini Morogoro.
Bw. Twaibu alielezea Wanahabari kwa kusema Mamlaka ilianzishwa na Serikali kama chombo cha utekelezaji wa majukumu ya Serikali kwa niaba ya Serikali chini ya uangalizi wa Serikali na kuwa na mfumo unaonesha utekelezaji wa majukumu kwa ufanisi zaidi. Kama ilivyo kwa Mamlaka Serikali nyingine nchini, lengo la kuanzishwa TAWA ni kutekeleza majukumu ya Idara ya Wanyamapori hasa ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini. Majukumu ya TAWA ni kusimamia shughuli za utawala, ulinzi, usimamizi wa raslimali ya Wanyamapori katika maeneo yote nje ya Hifadhi za Taifa na Hifadhi ya Ngorongoro.

Wandishi wa Habari walitaka kupata kauli ya TAWA na Wizara ya Maliasili na Utalii kuhusu ujenzi wa mradi wa uzalishaji umeme wa Stiglers Gorge uliyoko ndani ya Pori la Akiba Selous, kama TAWA na Wizara wanasemaje?


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa