Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI imesema hivi sasa inatoa sh. bilioni 22.2 kila mwezi ili kuboresha elimu ya msingi na sekondari hapa nchiKauli
hiyo imetolewa (Jumamosi, Septemba 2, 2017) na Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bw. George Simbachawene wakati akizungumza na
wahitimu 166 wa darasa la saba wa shule ya msingi ya Martin Luther,
kwenye sherehe za mahafali ya 10 zilizofanyika shuleni hapo katika
Manispaa ya Dodoma.
Waziri
Simbachawene ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali kwa niaba ya
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alisema Serikali itaendelea kuboresha elimu
ya sekondari kwa kuajiri walimu wengi zaidi wa masomo ya sayansi.
“Wazazi
wa wanafunzi wanaohitimu tunawakaribisha kwenye shule za sekondari kwa
sababu zote zina walimu wa kutosha, madawati na vifaa vya kufundishia.
Kila mwezi tunatenga sh. bilioni 22.2 kuendesha shule za msingi na za
sekondari hadi kidato cha nne,” alisema.Alisema hivi sasa, baadhi ya
shule zinakabiliwa na changamoto ndogo ya upungufu wa walimu wa sayansi
lakini nayo itatuliwa hivi karibuni kwa sababu vibali vya ajira vimeanza
kutolewa.
“Tunaendelea
kuziboresha na tumeshuhudia miaka ya karibuni wanafunzi bora kitaifa
wakitoka katika shule za Serikali ambazo wengi wamezoea kuziita ni shule
za kata. Hakuna shule za kata. Zote ni zimejengwa na Serikali,”
alisisitiza.“Ukienda vyuo vikuu, wanafunzi na ufaulu wa juu wengi wao ni
wale waliotoka kwenye shule za Serikali,” aliongeza.
Aliwataka
wanafunzi wanaojiandaa kufanya mitihani yao Septemba 6 na 7, wasiwe na
hofu kwani kufanya hivyo ni chanzo cha kuwafanya wachanganye mambo na
kisha kufeli.Kwa upande wake, Mkurugenzi wa shule hiyo, Bw. Rabbiely
Mmanga aliwaasa wazazi na kuwaomba wasiwaingize watoto kwenye migogoro
kwani matendo hayo yanawajisi watoto na kuwaathiri kisaikolojia hata
wawapo shuleni.
“Ninawaomba
sana wazazi, tofauti zenu ziishie chumbani na zisifike masikioni mwa
watoto kwa sababu zinawasumbua kisaikolojia na kuwaharibia concentration
yao kimasomo. Tumewahoji baadhi na wamesema wanaumia kwa kukumbuka adha
ambayo mama anaipata kutoka kwa baba, au baba anaipata kutoka kwa
mama,” alisema.
Katika
mahafali hayo, wanafunzi mbalimbali walipewa vyeti kwa kufanya vizuri
kwenye masomo mbalimbali huku Ismail Milambo na Nise-Magreth Malila
wakiibuka kidedea kwenye masomo yote (best academic performers). Tuzo za
nidhamu bora (discipline) zilichukuliwa na Michael Nyalusi na Sayuni
Kampuni.
Wanafunzi
wengine waliopata tuzo na masomo yao kwenye mabano ni Ismail Milambo
(Hisabati), William Terry William (Kiingereza), Majaliwa K. Majaliwa
(Sayansi), Nise Malira (Kiswahili), Clinton Dotto (Social Studies) na
Justin Kilimali (Kompyuta).
Wengine
walipewa tuzo kwenye vipengele vya michezo, uchoraji na sanaa, usafi,
uongozi shuleni, uimbaji na uongozi wa ibada.Katika risala yao,
wanafunzi wanaohitimu walisema wanaamini misingi ya elimu walioipata
kwenye shule ya Martin luther haitapotea bure na wakaahidi kufanya
mitihani yao kwa umakini ili watoke na ufaulu wa hali ya juu.
Wanafunzi wa darasa la saba kote nchini, wanatarajiwa kufanya mitihani yao ya kitaifa Septemba 6 na 7, mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment