Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga, akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu kuhusu hatua zinazochukuliwa katika ulindaji wa miundombinu ya barabara wakati walipokagua barabara ya Dodoma – Mayamaya iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Moshi Kakoso akitoa maoni kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga, juu ya ulindaji wa miundombinu na kuzingatia usalama wa mazingira wakati walipokagua barabara ya Dodoma – Mayamaya iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga, (watatu kushoto), akiwaonesha kingo za barabara baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakati walipokagua barabara ya Dodoma – Mayamaya iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami, mkoani Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga (katikati), wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakitoka kukagua daraja la Kelema linalounganisha Wilaya ya Chemba na Kondoa, mkoani Dodoma. Daraja hilo limekamilika kwa asilimia 98.
Serikali
imetakiwa kuweka mkakati wa kuzilinda, kutunza na kuhifadhi barabara
zote zinazojengwa kwa kiwango cha lami nchini ili kuziwezesha kudumu kwa
muda uliokusudiwa na hivyo kuepuka gharama za ukarabati wa mara kwa
mara.
Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu mheshimiwa Moshi
Suleman Kakoso amesema hayo mara baada ya kukagua barabara ya Dodoma –
Babati yenye urefu wa kilomita 263, ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha
lami umekamilika.
“Hakikisheni
ujenzi wa barabara unaendana na uboreshaji wa huduma na maisha ya
wananchi sehemu ambapo barabara hizo zinapita ili kuchochea maendeleo”,
amesema mheshimiwa Kakoso.
Makamu
mwenyekiti huyo amesema Kamati yake imeridhishwa na hatua zilizofikiwa
za ujenzi wa barabara Dodoma –Babati KM na daraja la Kelema
linalounganisha Wilaya za Chemba na Kondoa ambalo litawezesha barabara
hiyo kupitika kwa uhakika wakati wote.
“Nimefurahishwa
na taarifa aliyoitoa Meneja mradi wa barabara hii kwamba pamoja na
kujenga barabara pia mkandarasi amechimba visima vya maji katika maeneo
haya kwa ajili ya kusaidia wananchi jambo ambalo ni jema na la kuigwa na
makandarasi wengine”, amesisitiza Makamu Mwenyekiti Kakoso.
0 comments:
Post a Comment