Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua majengo yaliyo karabatiwa na serikali katika sekondari ya mpwapwa.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua jiko la kisasa linalo jengwa.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na wanafunzi wa Mpwapwa sekondari.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Kamati ya ujenzi wa Mpwapwa sekondari.
Baadhi ya madarasa ya Mpwapwa sekondari yaliyo karabatiwa.
VIONGOZI
wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wameishukuru serikali kwa kukarabati
sekondari ya Mpwapwa ambayo majengo yake yalikuwa yana hali mbaya.
Viongozi
hao wametoa shukrani hiyo mbele ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi
Mhe. Selemani Jafo alipokuwa katika ziara ya kikazi kukagua ukarabati
wa shule hiyo.Shule
hiyo ni miongoni mwa shule 88 kongwe zinazokarabatiwa na serikali
ambapo katika awamu ya kwanza ukarabati umeanza kwa shule 43.
Katika
shule hiyo, Serikali imefanikiwa kujenga bweni moja jipya la wasichana,
ukarabati wa mabweni 12 ya wavulana, ukarabati wa vyumba vya madarasa
22, bwalo la chakuka pamoja na jiko, maktaba, maabara tatu, ofisi za
walimu, mfumo wa maji na umeme ambapo jumla ya sh.bilioni 1.2
zimetumika.
Akizungumza
na viongozi katika ziara yake,Naibu Waziri Jafo ameipongeza Kamati ya
ujenzi kwa kufanyakazi bila kuchoka na kufanikisha kuibadili kabisa
shule hiyo ambayo kwasasa imegeuka kuwa shule bora ya kisasa tofauti na
ilivyokuwa awali.
Naibu
Waziri Jafo amewataka wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii kwani
serikali ya Dk. John Magufuli imeamua kuboresha miundombinu pamoja na
vifaa vya kutolea elimu kwa lengo la kufanikisha elimu bora hapa nchini.
0 comments:
Post a Comment