Home » » KATIBU MKUU MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO BIBI SIHABA NKING AFUNGUA MKUTANO WA MKUU WA MWAKA KWA MAAFISA WA USTAWI WA JAMII NCHINI MJINI DODOMA

KATIBU MKUU MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO BIBI SIHABA NKING AFUNGUA MKUTANO WA MKUU WA MWAKA KWA MAAFISA WA USTAWI WA JAMII NCHINI MJINI DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga akisikiliza Maelezo kutoka kwa washiriki tofauti wa Mkutano Mkuu wa Maafisa Ustawi wa Jamii nchini katika moja ya eneo la maonesho ya masuala yahusuyo Ustawi wa Jamii wakati wa Ufunguzi wa Mkutano huo uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi akipokea moja ya kitabu kinachoelezea masuala mbalimbali ya Ustawi wa Jamii kutoka kwa mshiriki wa Mkutano Mkuu wa Maafisa wa Ustawi wa Jamii nchini wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa wa Ustawi wa Jamii nchini uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa TASWO Dkt. Zena Mabeyo akitoa salamu za wananchama wa TASWO kwa mgeni rasmi Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(kulia waliokaa) wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa wa Ustawi Jamii nchini uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Mkurugenzi wa Taasisi ya JSI Dkt.Tuli Tuhuma akitoa maelezo kuhusu kazi za Taasisi yake kwa mgeni rasmi Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(kulia waliokaa) katika kuleta ufanisi wa kazi za Ustawi wa Jamii nchini wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa Ustawi wa Jamii nchini uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii Dkt. Abu Mvungi akitoa mada kuhusu umuhimu wa Maafisa Ustawi wa Jamii nchini wakati wa Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa hao uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(kushoto) akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa TASWO Dkt. Zena Mabeyo(kulia) wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa Ustawi wa Jamii nchini uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga akizungumza na Maafisa Ustawi wa Jamii nchini kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Maafisa hao uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Baadhi ya Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Serikalini na Taasisi na Mashirika yasiyo ya kiserikali wakimsikiliza Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(hayupo pichani) wakati akizungumza nao kabla ya kufungua wa Mkutano Mkuu wa Maafisa hao uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(wa pili kulia waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Ustawi wa Jamii nchini mara baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Maafisa  hao uliofanyika UDOM Mjini Dodoma.Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa