Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
ASKOFU wa Kanisa la The Gospel Ministry, Kanda ya Kati, Christopher
Madole, amekemea wabunge kutumia muda wao kuzomeana na kutukanana
badala ya kujadili hoja.
Akizungumza na Tanzania Daima jana juu ya mwenendo wa Bunge,
alisema inasikitisha kuona wabunge badala ya kujadili hoja wanajikita
katika malumbano ambayo hayawasaidii Watanzania.
Alisema kwa sasa umeanzishwa mtindo wa baadhi ya wanasiasa au jamii
kutumia mitandao ya kijamii kuchafuana, jambo ambalo linatia aibu
katika jamii.
“Sawa kwa sasa ni kipindi cha utandawazi, lakini inasikitisha kuona
mitandao ya kijamii ikitumiwa vibaya kwa kuweka picha za viongozi
wakiwa watupu, jambo ambalo ni aibu kwa taifa,” alisema.
Akizungumzia maadili ya Kitanzania, Askofu Madole alisema serikali
inatakiwa kuwa macho katika kudhibiti mambo ambayo hayapendezi katika
jamii, ikiwa ni pamoja na kuwapa onyo kali wale wote ambao wanatumia
vibaya mitandao ya kijamii
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment