MAWAKILI WA SERIKALI WANOLEWA MBINU ZA KISASA MIRADI YA UBIA
Mafunzo hayo yameandaliwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wakufunzi kutoka kampuni ya Cybiant kutoka nchini Malaysia yamefungwa rasmi tarehe 6 Februari, 2026 Jijini Dodoma.
Akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga katika kuwaongezea uwezo mawakili hao kuhusiana na mbinu za kisasa za majadiliano (negotiations), uchambuzi wa mikataba, ununuzi na utiaji saini wa mikataba, usimamizi wa mikataba na namna bora ya kupata taarifa za miradi mikubwa ya maendeleo.
“Mafunzo haya ni nyenzo muhimu kwa Mawakili wa Serikali kuhakikisha kuwa Miradi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi inakuwa na tija na inayolinda rasilimali za nchi.” Amesema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Aidha, Mhe. Maneno ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa Mawakili wa Serikali ili kuhakikisha kuwa miradi mbalimbali inayoingiwa kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi inaendana na utekelezaji wa Dira 2050.
“kupitia mafunzo haya tunaamini kuwa tutapata Mawakili wenye weledi na ubora mkubwa katika kutengeneza mikataba ya miradi mikubwa itakayosaidia kutengeneza mazingira rafiki ya uwezekezaji kuelekea utekelezaji wa Dira 2050”.Amesema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Kwa upande wake, Wakili wa Serikali Bw. Ildephonce Mukandara kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo ameushukuru uongozi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuwezesha kufanyika kwa mafunzo hayo ambayo yatawasaidia kuongeza ujuzi katika Upekuzi wa Mikataba ya Ubia na kuisaidia Serikali katika utekelezaji wa Dira 2050.
Mafunzo hayo ni mwendelezo
wa mikakati ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakikisha kuwa Watumishi wake wanaongeza ujuzi utakaowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao.
TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHMINI (M&E) ASA YAPIGWA MSASA
Mafunzo hayo yamefunguliwa rasmi na Mtendaji Mkuu wa ASA, Bw. Leo Mavika, ambaye amewasisitiza washiriki kuyazingatia kikamilifu ili kuyaweka katika vitendo na hivyo kuisaidia Taasisi kufikia malengo yake ya kimkakati.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Bw. Mavika amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa timu ya M&E katika kusimamia na kupima utendaji wa Taasisi, kuhakikisha thamani ya fedha kwenye miradi, kufuatilia mwelekeo wa utekelezaji wa miradi pamoja na usimamizi wa bajeti ya ASA.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) cha ASA, Bw. Emmanuel Maziku, amesema mafunzo hayo ni nyenzo muhimu katika kuimarisha uwezo wa kufuatilia na kutathmini utendaji wa Taasisi, usimamizi wa kazi za Wakala pamoja na miradi inayotekelezwa.
Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatawajengea washiriki uwezo wa kufanya ufuatiliaji na tathmini ya majukumu ya idara, vitengo na mashamba ya ASA, hatua itakayochochea na kukuza ufanisi na uwajibikaji ndani ya Taasisi.
Serikali Yabainisha Maeneo ya Miradi ya Umeme wa Upepo na Jua, Kishapu kuzalisha MW 150
Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Februari 05, 2026 bungenini jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mwera, Mhe. Suleiman Mohamed Rashid aliyehoji juu ya mpango wa Serikali wa kutumia vyanzo vya umeme na upepo juu vilivyopo nchini.
" Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 150 katika Wilaya ya Kishapu, Shinyanga ambapo awamu ya kwanza ya mradi huo wenye megawati 50 imekamilika na hatua za kuingiza umeme huo katika Gridi ya Taifa zimeanza," Amesema Mhe. Salome.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe Esther Malleko aliyehoji mkakati wa Serikali katika kumaliza usambazaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyosalia mkoani humo, Mhe. Salome amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na kazi za utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro ambapo hadi kufikia Januari 2026 jumla ya vitongoji 2,032 kati ya 2,258 sawa na asilimia 90 vilipatiwa umeme na kusalia vitongoji 226 ambavyo vitapelekewa umeme kupitia miradi mbalimbali.
MCHENGERWA: SERIKALI IMEDHAMIRIA KUBORESHA MAISHA YA WALIMU NCHINI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema Serikali sikivu ya Awamu ya Sita imejidhatiti katika kuboresha maisha ya walimu nchini, hususani katika maeneo ya maslahi na mazingira ya kazi.
Mhe. Mchengerwa amesema hayo wakati akizungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Wilaya ya Rufiji, mara baada ya walimu hao kufanya uchaguzi wa viongozi uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Maendeleo Ikwiriri.
“Tumedhamiria kuboresha maisha yenu. Binafsi, tangu nikiwa Waziri wa UTUMISHI hadi sasa nikiwa Waziri wa TAMISEMI, nimekuwa mstari wa mbele kupigiania madaraja yenu na maslahi ya walimu kwa ujumla amesisitiza.
Aidha, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa Taifa lina bahati ya kuwa na Rais anayewajali na kuwathamini walimu na kwani baada ya kupokea ombi la kuwapandisha madaraja walimu, Rais hakusita kulitekeleza, licha ya ukweli kuwa hatua hiyo ilisababisha ongezeko katika bajeti ya mishahara.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Pwani, Bi. Susan Shesha, amemshukuru Waziri Mchengerwa kwa juhudi zake za kupigania maslahi ya walimu tangu akiwa Waziri wa UTUMISHI, na kueleza kuwa katika nafasi yake ya sasa kama Waziri wa TAMISEMI, ameendelea kutoa kipaumbele kwa walimu kwa kusimamia miradi ya elimu kwa uadilifu, ili kuhakikisha kuwa inawanufaisha wananchi kwa ujumla.
DENMARK KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA
Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma
Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu – El Maamry Mwamba, amefanya mazungumzo na ujumbe kutoka Danish Public Investment Fund for Development Countries (IFU), ukiongozwa na Balozi wa Denmark Nchini, Mhe. Jepser Kammersgaar, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dodoma.
Mazungumzo yao yalilenga kujadili fursa mbalimbali zikiwepo za mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za maji na nishati.
Aidha, kupitia Mfuko huo Tanzania inaweza kunufaika na aina mbalimbali za ufadhili unaotolewa na Mfuko huo ikiwemo uwekezaji wa hisa (equity investment), na dhamana (guarantees).
Kikao hicho kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa IFU, anayeshughulikia Sekta ya Umma katika Mikopo Nafuu na Misaada, Bi. Tina Kollerup Hansen, na Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Dhamana, Bw. Theo Ib Larsen.
Kwa upande wa Wizara ya Fedha kikao hicho kilihudhuriwa na Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje, Bw. Melckzedeck Mbise na Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Bi. Tiba Kisonga.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
COSTECH WAKABIDHI RASMI ENEO LA MRADI KWA MKANDARASI KWA AJILI YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA STI JIJINI DODOMA
TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imekabidhi rasmi
eneo la mradi kwa mkandarasi TIL Construction Limited kwa ajili
ya kuanza ujenzi wa jengo jipya la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu
(STI) jijini Dodoma.
Akizungumza baada ya kukabidhi eneo hilo la mradi
Machi 25,2025 jijini Dodoma Mratibu Msaidizi wa Mradi
wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET)
kutoka COSTECH, Dkt. Aloyce Andrew, amesema hatua hiyo
inalenga kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau wa taasisi hiyo.
WMA YAELEZA MAFANIKIO YAKE IKIWEMO KUAJIRI WAFANYAKAZI 186
NSSF YATOA ELIMU YA SKIMU YA TAIFA YA HIFADHI YA JAMII YA SEKTA ISIYO RASMI ILIYOBORESHWA KWA KAMATI YA BUNGE
MRITHI WA KINANA KUPATIKANA JANUARI HII
Na Dotto Kwilasa, JamhuriMedia, Dodoma
BAADA ya kimya cha muda mrefu kuhusu nani anachukua nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM) jibu limepatikana ambapo anatarajiwa kupatikana kati ya January 18 au 19 mwaka huu.
Hatua hii ni mara baada ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Abdulrahman Kinaana kutangaza kustaafu kwenye nafasi hiyo tangu Julai mwaka jana kwa madai ya kutaka kupumzika ambapo Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan aliliridhia ombi lake.

Akizungumza leo Januari 7,2025 Jijini Dodoma, Katibu wa NEC,Itikadi , Uenezi na Mafunzo wa Chama hicho Amos Makala ameeleza kuwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti huwa haigombewi wala kujazwa fomu bali hutokana na mapendekezo ya Mkutano Mkuu na halmashauri kuu ya CCM.
“Niwaombe wanachama watu kuachana na taharuki zinazoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mrithi wa Makumu Mwenyekiti wa chama Abdulahman Kinana, nafasi hii haigombewi ila inapendekezwa, ” ameeleza Makala.
Makala amewaambia waandishi wa habari kuwa kwa sasa hakuna mchakato wowote wa mrithi wa nafasi hiyo ambaye atapatikana baada ya mapendekezo ya jina katika kikao cha Kamati kuu na Halmashauri kuu Taifa.
%20NSSF.jpg)














.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)







