Home » » MWENYEKITI WA CCM MKOA WA DODOMA AMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU 28 KWA KUTEMBELEA WILAYA ZOTE 7 MKOANI HAPO.

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA DODOMA AMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU 28 KWA KUTEMBELEA WILAYA ZOTE 7 MKOANI HAPO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Alhaj Adam Kimbisa wa kwanza kulia na Mwenyekiti wa ccm wilaya ya kondoa anaefuatia kutoka kulia wakisikiliza burudani za vikundi mbambali wakati wa ziara yake wilayani Kondoa
Kushoto ni Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Dodoma Alhaj Adam Kimbisa, akifuatiwa na Mbunge wa Kondoa kaskazini wakicheza ngoma ya asili ya warangi wilayani Kondoa wakati wa ziara ya siku mbili ya mwenyekiti huyo wa CCM mkoa wa Dodoma.
Jembe la sera CCM, Haji Manara akiwaweka sawa wananchi wa kijiji cha Kinyasi wilayani Kondoa kabla ya mwenyekiti CCM mkoa kuwahutubia wananchi hao wakati wa ziara yake ya siku mbili wilayani humo,iliyoanza juzi na kumalizika jana.
Mkuu wa wilaya ya Kondoa Omary Kwaang' akisikiliza kwa makini moja kati ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na wananchi wa kijiji cha Kinyasi kuhusiana na mgogoro wa Ardhi na mipaka kati ya wananchi na serikali.




Na. Bilson Vedastus - Dodoma

Hatimaye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Dodoma Alhaji Adam Kimbisa amehitimisha ziara yake ya zaidi ya siku 28 kutembelea wilaya saba za mkoa wa Dodoma kwa lengo la kukagua na kuimarisha uhai wa chama kwa kipindi cha miaka minne kabla ya kuelekea uchaguzi mkuu huku akiahidi kutatua migogoro mbalimbali ikiwemo  mgogoro wa mpaka kati ya hifadhi ya Mkungunero na Ardhi inayotumiwa na wananchi wa vijiji kumi vinavyozunguka hifadhi hiyo iliyopo kata ya Kinyasi wilayani Kondoa mkoani Dodoma

Akiwa wilayani Kondoa Alhaji Kimbisa  amesema atazungumza na viongozi wa idara husika pamoja na kumuona waziri mkuu mheshimiwa Mizengo Pinda ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya mgogoro huo
Aidha Alhaji Kimbisa aliwaomba wananchi kuwa watulivu wakati ccm wakifanyia kazi mgogoro huo wakishirikiana na mkuu wa wilaya hiyo ili kupata haki ya pande zote mbili.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kondoa Omary Kwaang amekiri kuwepo kwa mgogoro huo ambao umedumu tangu mwaka 2006 baada ya wataalamu kuanza kupima hali ambayo mwaka 2007 ilisababisha askari kuuwawa ambapo amesema zaidi ya mara mbili kwa barua na maongezi ya ana kwa ana viongozi wa wilaya ya kondoa wamelifikisha swala hilo kwa vyombo husika ikiwemo wizara ya Ardhi,Tamisemi na serikali kuu lakini hadi leo hakuna ufumbuzi wowote juu ya tatizo hilo

Mmoja wa waathirika wa mgogoro huo kwa upande wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Ramadhan Ally akizungumza na Nyemo fm habari alisema chanzo cha mgogoro huo ni kubadilishwa kwa mipaka iliyowekwa tangu enzi za mwalimu Nyerere ambapo sasa serikali imebadilisha mipaka hiyo na kusababisha  kuingilia haki ya wananchi hao.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma,Adam Kimbisa kabla ya kuzungumza na hadhara ya wananchi alikaa na wazee wa kondoa mjini ambao katika maongezi wao walilalamikia uhaba wa maji na kusema hali hiyo inakwamisha maendeleo yao kwa ujumla.

Wazee hao pamoja na vingozi wa dini mbalimbali walifikisha malalamiko hayo siku moja kabla ya mwenyekiti kufanya mkutano wa hadhara wilayani Kondoa uliohusisha kata za Chemchem,Kondoa mjini na Kilimani wakati walipokuwa wakizungumza nae ndani ya ukumbi wa CCM wilayani Kondoa.

Mbunge wa jimbo hilo la Kondoa Kaskazini Zabeini Mhita pia alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na kwamba tayari hatua za mwanzo zinaendelea ambapo amewasilisha bungeni mahitaji ya fedha zitakazosaidia kuondoa miundombinu mobovu na iliyochakaa sambamba na kusambaza miundombinu mipya ili kuondoa tatizo hilo.
Hata hivyo Zabein amesema serikari inatakiwa kutambua kuwa kuna ongezeko la watu ndani ya wilaya hiyo kwani inakuwa na watu wanazaliwa hivyo ni vema kukapanuliwa miundombinu ya maji iatakayoendana na ongezeko la watu.

Aidha mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma akikamilisha ziara yake ya siku mbili kwa kila jimbo mkoani Dodoma akianzia wilaya ya Mpwapwa,Kongwa,Chamwino,Dodoma mjini,Bahi,Chemba na kutamatisha na Kondoa amesema atahakikisha anashugulika ili kutatua kero za wananchi kadri ya uwezo wake kwa kushirikiana na idara husika ndani ya serikali bila kujali itikadi za dini, vyama vya siasa na ukabila.

Alihaji Adam Kimbisa katika ziara yake ndani ya wilaya ya Chemba na Kondoa aliambatana na Katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Dodoma Donard Simango Mejitii,aliyewahi kuwa Katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Dar es salaam Haj Manara, Mbunge wa jimbo la Kondoa kaskazini Zabein Mhita, Mkuu wa wilaya ya Kondoa na viongozi mbalimbali wa Chama cha mapinduzi CCM na serikali.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa