Waziri
wa Fedha Saada Mkuya Salum (kushoto) akibadilishana hati ya mkataba wa mkopo
uliotolewa na Serikali ya Japani kwa Tanzania, hafla hiyo ilifanyika leo mjini
Dodoma. Kulia ni Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada.
Waziri
wa Fedha Saada Mkuya Salum (wa kushoto) akiongea na waandishi wa habari pamoja
na Maafisa kutoka Wizara ya Fedha (hawapo pichani) wakati wa kutiliana saini
mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa Tanzania. Hafla hiyo
ilifanyika leo mjini Dodoma. Kulia ni Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki
Okada.
Balozi
wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada akiongea na waandishi wa habari pamoja na
Maafisa kutoka Wizara ya Fedha (hawapo pichani) wakati wa kutiliana saini
mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa Tanzania katika hafla
ilifanyika leo mjini Dodoma.
Mwakilishi
wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japani (JICA) nchini Yasunori Onioshi
akiahidi shirika lake kuendelea kushirikiana na Serilkali ya Tanzania katika
masuala mbalimbali yamaendeleo nchini, leo mjini Dodoma.
Baadhi
ya waandishi wa habari pamoja, Maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Ubalozi wa
Japani wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Fedha
Saada Mkuya Salum wakati wa kutiliana saini mkataba wa mkopo uliotolewa
na Serikali ya Japani kwa Tanzania katika hafla ilifanyika leo mjini Dodoma.
(Picha
na habari na Ingiahedi Mduma na Eleuteri Mangi-Wizara ya Fedha)
TANZANIA YAPATA
BILIONI 24.1 KUSAIDIA BAJETI YA SERIKALI
Serikali
ya Tanzania imepokea shilingi bilioni 24.1 kutoka Serikali ya Japani kwa ajili
ya shughuli za maendeleo hapa nchini.
Akizungumza katika hafla hiyo ya kutiliana saini , Waziri wa Fedha Sada Salum Mkuya aliishukuru Serikali ya Japani kwa kuwa na ushirikiano mzuri na Tanzania.
“Mkopo
huu utachangia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2014/2015, na fedha hizo
zitaelekezwa katika sekta ya Maji, Elimu na Afya” alisema Waziri Mkuya.
Mkuya
aliishukuru Serikali ya Japani kwa misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikiitoa ambayo
imeleta mafanikio makubwa Tanzania.
Alisema kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ,misaada hiyo imesaidia kupunguza umaskini na kuongeza kipato kwa wananchi.
Akijibu
swali kuhusu fedha hizo za mikopo kuchelewa kufika, Waziri Mkuya alisema kuwa changamoto
kubwa ambayo Serikali imekuwa ikiipata ni kutokana na taratibu za sera za nchi husika ambapo kila nchi wana
sera zao.
Kwa upande wake Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada alisema kuwa msaada huo unahusiana na ushirikiano wa pamoja na Benki ya Dunia katika mkopo wa kumi na moja wa kusaidia kupunguza umaskini ambao umekuwa ukitolewa tangu mwaka 2001.
Mikopo hiyo imekuwa ikitolewa kwa masharti ya mkataba wa mkopo nafuu wa riba ya asilimia 0.01 kwa Serikali hapa nchini.
Balozi Okada alisema kuwa nchi yake imekuwa ikitoa mikopo mabalimbali ili kusaidia Serikali ya Tanzania katika kupunguza umaskini ambapo misaada hiyo imekuwa ikitumika kufuatana na GBS hapa Tanzanaia kwa kutoa fedha moja kwa moja ambazo zinalenga kuharakisha juhudi za kupunguza umasikini hususani MKUKUTA.
Naye Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA) nchini Yasunori Onioshi alisema kuwa shirika lake litaendelea kushirikiana na Serilkali ya Tanzania katika kusaidia bajeti yake kwani Tanzania inakua kwa haraka na mahitaji yake yanaendelea kuongezeka kila mara.
Makampuni ya Kijapani yanayofanya kazi na Serikali ya Tanzania ni pamoja na Kampuni ya Sigara (TCC) inayomilikiwa na Kampuni ya Kimataifa ya Tumbaku ya Kijapani, Panasonic Energy Tanzania na JICA.
Hali
ya hewa ya Dodoma ni baridi na majadiliano kuhusu Bajeti ya Serikali yameanza
na yanaendelea.
Imetolewa na:
Msemaji Mkuu
Wizara ya Fedha
16/06/2014
0 comments:
Post a Comment