Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Chuo kikuu cha Dodoma
Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) umelipa madeni ya zaidi ya Sh.
milioni 63 ikiwa ni malipo ya kusimamia mitihani ya muhula uliopita ya
wahadhiri wa Shule ya Sanaa na Sayansi za Jamii waliogoma na kukwamisha
mitihani ya muhula huu iliyotakiwa kuanza mapema wiki hii.
Kaimu
Mkuu wa Shule hiyo, Dk. Frowing Nyoni, alisema kuwa awali, hawakuwa na
fedha za kulipa deni hilo, lakini wamehakikisha wanapambana mpaka fedha
hizo zikapatikana.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanataaluma wa Chuo
hicho (Udomasa), Mhadhiri Msaidizi Paulo Loisulie, na Rais wa Serikali
ya Wanafunzi wa Shule hiyo, Masatu Kyabwene, walithibitisha pande hizo
mbili kufikia suluhu na kwamba, mitihani iliendelea kama kawaida.
Hata
hivyo, hivi karibuni kulielezwa kuwapo kuvurugwa mitihani mitatu,
ambayo ilifanywa chini ya usimamizi wa wahadhiri, ambao siyo waliotakiwa
kufanya kazi hiyo kufuatia waliostahili kuwa katika mgomo ambambo
iliyotakiwa kufanywa na wanachuo wa mwaka wa tatu iligawiwa kwa wale wa
mwaka wa kwanza, huku mtihani mmoja wa lugha (Literature) uliotakiwa
kufanywa kwa kutumia vitabu wanachuo wakizuiliwa kutumia na hivyo
kusababisha malalamiko.
Mhadhiri Msaidizi anayefundisha na
aliyestahili kusimamia somo hilo, Honoratha Thomas, akizungumzia tatizo
hilo amesema wameafikiana mitihani yote mitatu iliyofanywa bila
usimamizi wa wahusika isitambuliwe.
Hata hivyo, Dk. Nyoni
alikataa kuzungumzia suala hilo akisema kwa kuwa bado wanalifanyia
uchunguzi na kwamba ikibainika kulitokea matatizo, kuna hatua
zinazotakiwa kufuatwa ili kuweka mambo sawa na kutaja hatua hizo kuwa ni
pamoja na mitihani kurudiwa kutungwa upya au wanachuo kufanya katika
muhula ujao kama mitihani maalumu.
Home »
» UDOM YALIPA DENI LA SHS. MILIONI 63 ikiwa ni malipo ya kusimamia mitihani ya muhula uliopita ya wahadhiri wa Shule ya Sanaa na Sayansi za Jamii waliogoma na kukwamisha mitihani ya muhula huu iliyotakiwa kuanza mapema wiki hii
0 comments:
Post a Comment