Home » » PINDA AITWISHA MZIGO NEC

PINDA AITWISHA MZIGO NEC

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hatima ya upigaji wa kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa itatokana na tathmini itakayofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuona jinsi hatua hiyo ilivyotekelezwa katika Mkoa wa Njombe.
Pinda aliyasema hayo jana nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya waandishi wa habari kutaka kujua msimamo wa serikali juu ya tarehe ya kupiga kura.
Alisema Serikali imekwisha kutoa asilimia 70 ya fedha za kununulia mashine 8,000 za Biometric Voters Registration (BVR) zitakazotumika katika uandikishaji huo.
Alisema uandikishaji nchi nzima unatarajiwa kuanza mapema Aprili na kila kata zitawekwa mashine mbili hadi tatu.
“Tukianza uandikishaji nchi nzima ndiyo tutaona changamoto zaidi zipo wapi na zinaweza kutupeleka katika uamuzi wa aina gani. Ila hilo litakuwa jukumu la tume (NEC), sisi kazi yetu ni kuhangaika BVR zinazotakiwa ziwe zimepatikana kwa wakati.
“Tume ndiyo inaweza kulizungumzia suala hilo kwa undani. Unajua inatakiwa mpaka kufikia Aprili 28 mambo yote yawe yamekamilika na siku mbili baadaye (Aprili 30) ndiyo siku ya kura. Kama wanasema mwezi mmoja ni sawa, tunaweza kuendelea na mambo mengine huku elimu ikitolewa kwa wananchi.
“Tulichojifunza ni kwamba katika maeneo ya mijini (Makambako na Njombe Mjini), tukianza uandikishaji nchi nzima ni lazima maeneo kama hayo tuyape nafasi kubwa zaidi tofauti na vijijini,” alisema.
Chanzo:Mtanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa