Home » » . Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete Afungua kikao cha kuipitia Ilani ya Uchaguzi wa 2015, mjini Dodoma leo

. Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete Afungua kikao cha kuipitia Ilani ya Uchaguzi wa 2015, mjini Dodoma leo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Mrisho Kikwete akionyesha kitabu ya Rasimu ya Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, wakati wa Kikao cha Kamati Kuu cha kuijadili na kuipitisha Ilani hiyo kinachofanyika, leo Julai 4, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wakipitia Rasimu ya Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, wakati wa Kikao cha Kamati Kuu cha kuijadili na kuipitisha Ilani hiyo kinachofanyika, leo Julai 4, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma.
 Katibu Mkuu Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza wakati akimuomba Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Mrisho Kikwete kufungua Kikao cha Kamati Kuu cha kuijadili na kuipitisha Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kinachofanyika, leo Julai 4, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM Makao Makuu, Mjini Dodoma. Wengine pichani ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein (kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndg. Phillip Mangula.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakiwa kwenye Kikao hicho.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa