Na Tiganya Vincent, Dodoma
Wakala wa Vipimo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa inakusudia kuanzisha vituo
maalum vya ununuzi wa mazao ya wakulima (buying centres) katika
vitongoji nchi nzima ili kuondoa unyonyaji na ukandamizaji unaofanwa na
wachuuzi wa mazao ya wakulima.
Kauli
hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Viwanda,Biashara na
Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo
Mhe. Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni lini Serikali itasimamia sheria
kuondoa unyonyaji unaofanywa na wachuuzi wakati wa kununua mazao ya
wakulima.
Alisema
kuwa katika kutekeza hayo hakuna mfanyabiashara atakayeruhusiwa
kusafirisha mazao ambayo yamefungashwa kinyume kinyume cha Sheria ya
vipimo na kuongeza kuwa katika kusimamia jambo hilo vitaanzishwa vituo
maalum vya ukaguzi bila kusabaisha usumbufu katika ufanyaji biashara.
Mhe.
Mwijage amewaagiza Maafisa Ugani walioko vijijini watumike kusimamia
matumizi ya vipimo rasmi katika vituo hivyo na kutoa taarifa zote muhimu
kwa Wakala wa Vipimo.
Aidha
,alisema kuwa Serikali imeamua kufanyia mapitio Sheria ya Vipimo sura
340 ili kuondokana na unyonyaji na ukandamizaji unaofanywa na wachuuzi
wa mazao ya wakulima.
Alisema
kuwa Serikali imeamua kufanyia mapitio ya Sheria hiyo ili kuweka
mazingira mazuri kwa lengo la kumlinda muuzaji kwa kuwadhibiti manunuzi
wanaotumia njia za udandanyifu wakati wanaponunua mazao ya wakulima.
Mhe.
Mwijage alisema kuwa katika kipindi kifupi kijacho Serikali itawalisha
mabadiliko hayo bungeni ili ifanyiwe marekebisho yanayostahili.
Aidha
, Waziri huyo alisema kuwa pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vipimo
yanatarajia kufanywa , Wakala wa Vipimo imewasilisha Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mapendekezo ya kutungwa
kwa sheria ndogo(by laws) ili ziweze kuwaongoza wakulima na wafanyabiashara kufungasha mazao.
Mwisho
SERIKALI KUTOA MAFUNZO MAALUM YA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI
Na Tiganya Vincent, Dodoma
Wizara ya Fedha na Mipango imesema kuwa iko
tayari kutoa mafunzo maalum ya elimu ya fedha kwa wananchi wote
wakiwemo wakinamama kuhusu ili kuleta uelewa mpana wa upatikanaji wa
huduma za fedha na taratibu zinazohusu mikopo.
Kauli
hiyo imetolewa leo mijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango
Dkt. Ashatu Kachwamba Kajaji wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti
Maalum Mhe. Anna Lupembe aliyetaka kujua mipango ya Serikali ya kupeleka
huduma za kibenki vijijini ili wanawake waweze kupata mikopo.
Aidha,
alisema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Benki Kuu ya Tanzania
(BOT) imehakikisha kuwa huduma za kibenki zinawafikia wananchi wengi ili
kurahisisha shughuli zao mbalimbali za kiuchumi katika maeneo ya mjini
na vijiji.
Alisema
kuwa baadhi ya Benki zimeanzisha huduma za Kibenki kupitia mawakala, na
huduma za kifedha kupitia simu za mikononi ambazo zimewasaidia wananchi
kwenye sehemu ambako hakuna matawi ya Benki.
Mhe. Dkt.Kajaji aliongeza kuwa Wizara
ya Fedha na Mipango kupitia Benki Kuu inaendelea kuweka mazingira
wezeshi ili kusaidia nguvu za wananchi na sekta binafsi kuanzisha benki
au taasisi za fedha.
Alitoa
wito kwa wananchi kutumia fursa ya mazingira mazuri ya uwekezaji
yaliyopo hapa nchini kuzishawishi Benki kuanzisha huduma za kibenki
katika maeneo yao.
Mhe.
Dkt.Kajaji alisema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea
kushawishi Benki nchini kupanua shughuli zao ili ziwafikie wananchi
wengi hasa wale wa vijijini wakiwemo akina mama.
Aidha,
Naibu Waziri huyo alisema kuwa Serikali kwa kushirikiana na BOT iko
tayari kutoa mafunzo maalum ya elimu ya fedha kwa wananchi wote wakiwemo
wakinamama kuhusu utumiaji wa huduma za kifedha ili kuleta uelewa mpana
wa upatikanaji wa huduma za fedha na mikopo.
0 comments:
Post a Comment