Na: Lilian lundo – MAELEZO – Dodoma
Bunge
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limepitisha sheria ya
marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2016 ikiwemo kuanzishwa kwa
Mahakama ya Mafisadi.
Muswada
huo umewasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju
ambao ulikuwa na marekebisho ya sheria tano ambazo ni sheria ya mamlaka
za Mahakama ya Rufaa, sheria ya Makosa ya Uhujumi Uchumi, sheria ya
usimamiaji haki na matumizi ya sheria, sheria ya mahakama za mahakimu
pamoja na sheria ya rufaa za kodi.
“Ili
kutekeleza ahadi ya Serikali ya kuanzishwa Mahakama Maalum kwa ajili ya
kushughulikia makosa ya rushwa (ufisadi) na uhujumu uchumi, imeonekana
kuwa kuna umuhimu wa kurekebisha sheria hii kwa kuanzishwa Divisheni
Maalum ya Mahakama Kuu ambayo itakuwa na Majaji pamoja na watumishi
wengine ambao wanahusika moja kwa moja na kesi za rushwa na uhujumu
uchumi tu,” alifafanua Mhe. Masaju.
Mwanasheria
Mkuu aliendelea kwa kusema kuwa, makosa yatakayofunguliwa katika
mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ni yale ambayo
thamani yake haipungui shilingi bilioni moja, lengo la kuweka ukomo huo
kwa baadhi ya makosa ni kuiwezesha Divisheni hiyo kusikiliza makosa
makubwa ya rushwa na uhujumu uchumi na kuacha makosa madogo yasiyofikia
thamani hiyo kuendelea kusikilizwa mahakama za wilaya, hakimu mkazi au
mahakama kuu.
Aidha,
marekebisho mengine yanayopendekeza katika sheria hiyo ni pamoja na
kuboresha masharti ya kutoa dhamana pale kosa linapohusisha fedha au
mali ambayo thamani yake inazidi shilingi milioni kumi ambapo sheria ya
sasa inaeleza kuwa masharti ya dhamana kwa kosa
kama hilo ni kutoa fedha tasilimu (cash deposit) inayolingana na nusu ya
thamani ya mali ya kosa husika na thamani ya nusu inayobaki itolewe kwa
njia ya bond.
Muswada
unapendekeza kwamba masharti yaboreshwe ili pale mshtakiwa anapokuwa
hana fedha inayotakiwa mahakamani basi aruhusiwe kutoa mali hiyo na kama
mali hiyo haihamishiki basi hati au ushahidi unaothibitisha umiliki wa
mali hiyo utolewe Mahakamani.
Marekebisho
mengine ni pamoja na adhabu kwa makosa ya rushwa na uhujumu uchumi iwe
ni kifungo gerezani kisichopungua miaka 20 na kisichozidi miaka 30 au
vyote kwa pamoja.
0 comments:
Post a Comment