Na Fatma Salum- MAELEZO.
1/6/2016. Dodoma
Serikali
imeagiza kuwa kuanzia Mwezi Julai mwaka huu ni lazima mfumo wa
kielektroniki utumike katika utoaji wa risiti kwa tozo, faini, ada na
malipo mengine yote ya Serikali Kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa na
Wakala wote wa Serikali ili kudhibiti upotevu wa mapato.
Agizo
hilo limetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango
wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara
yake kwa mwaka wa fedha 2016/2017 leo Bungeni mjini Dodoma.
Dkt.
Mpango alisema kuwa agizo hilo pia linahusisha malipo ya faini za
mahakamani, faini za usalama barabarani, viingilio kwenye mbuga za
wanyama na vibali vya kuvuna maliasili.
“Naziagiza
ofisi zote za Serikali kutoa risiti za kielektroniki kwa malipo yote
yatakayofanyika kwani matumizi ya vifaa na mifumo ya kielektroniki
katika ukusanyaji wa mapato yataongeza ufanisi na kudhibiti upotevu wa
mapato ya Serikali.” Alisema Dkt. Mpango.
Katika
kufanikisha hilo Dkt. Mpango aliongeza kuwa Maafisa Masuuli wote
wanaelekezwa kusimamia ipasavyo utekelezaji wa agizo hilo.
Katika
hatua nyingine, Dkt. Mpango alisema kuwa Serikali imeamua kufanya
uthamini wa majengo kwa mkupuo ili kuongeza mapato yatokanayo na kodi ya
majengo na usimamizi wake utakuwa chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Katika
hotuba hiyo Dkt. Mpango amefafanua mkakati wa Wizara yake kusimamia
kikamilifu utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano
kuanzia 2016/17 hadi 2020/21 ambao umejikita katika kujenga msingi wa
uchumi wa viwanda na maendeleo ya watu.
0 comments:
Post a Comment