Home » » Familia zinakwamisha kesi za watoto kwa kuficha ushahidi- Dkt. Kigwangala

Familia zinakwamisha kesi za watoto kwa kuficha ushahidi- Dkt. Kigwangala


Na Godfriend Mbuya

Naibu Waziri wa Afya Ustawi wa Jamii Jinsia na Wazee na Watoto Dkt. Khamis Kigwangalla amesema Serikali itaendelea kutumia sheria zilizopo kwa ajili ya kutoa adhabu kwa wanaofanya vitendo vya udhalilishaji kwa watoto pamoja na kutoa elimu kwa jamii lakini siyo kuwahasi wanaume.

Dkt. Kigwangalla amesema hayo bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu CCM, Khadij Aboud aliyetaka kujua , pamoja na serikali kuwa sheria nyingi lakini bado watoto wamezidi kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji, na kuitaka serikali ieleze mkakati mbada wa kukabiliana na tatizo hilo.

' Serikali itaendelea kutoa elimu pamoja na kufuata sheria ya mtoto ya mwaka 2009 na sheria nyingine za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kukabiliana na matukio ya udhalilishaji wa watoto nchini” Amesema Dkt. Kigwangalla.

Ameongeza kuwa serikali haita wahasi wanaume wanaofanya vitendo hivyo badi itaendelea kutoa elimu juu ya madhara ya udhalilishaji kwa watoto na kuitaka jamii iwe mstari wa mbele katika kufichua na kukemea vitendo hivyo hususani kutoa ushirikiano wa kutosha inapotokea kesi kama hizo.

“Familia nyingi hazitoi ushirikiano wa kutosha kuhusu kesi za udhalilishaji wa watoto nchini kwa kuhofia kumpoteza ndugu yao kutumikia kifungo jambo linalokwamisha wahusika kupatikana na hatia kwa kukosa ushahidi wa kutosha” Amesema Kigwangalla.

Aidha Naibu Waziri amesema kuwa watoto ambao hufanyiwa vitendo hivyo husaidiwa kupata usaidizi wa kisaikolojia kutoka kwa wataalamu waliopo vituo vya afya pa,moja na ustawi wa jamii.

Wakati huo huo akikazia majibu hayo Waziri mwenye dhamana ya afya nchini Ummy Mwalimu amesema serikali ipo kwenye mchakato wa kuitaka mahakama,kutenga muda maalumu wa kusikiliza kesi za watoto ili ziweze kushughulikiwa kwa wakati.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa