Na GODFRIEND MBUYA
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Freeman Haikaeli
Mbowe ameiomba serikali mjini Dodoma itoe upendeleo kwa shule zote ambazo
wazazi wamejitahidi na kuanzisha mabweni kwa ajili ya kidato cha tano na sita ili
yaweze kukamilika.
Mbowe ameyasema hayo katika kipindi cha maswali na majibu
bungeni, ambapo ameiomba serikali isaidie wazazi ambao wameonyesha nia ili
shule hizo ziweze kufaidisha wengi.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa TAMISEMI Selemani Jaffo
amesema kutokana na umuhimu wa elimu na namna ambavyo baadhi ya wazazi
wamejitoa ni lazima serikali itafanya linalowezekana kuweza kuwaunga mkono.
“Tutaweka kipaumbele katika eneo hilo na ushauri wako ni
mzuri kwetu , na kweli kuna maeneo ambayo nimepita na kujionea na tunawapongeza
wazazi wote wanaojenga mabweni ili wanafunzi wanaofaulu wasikose sehemu za
kusomea na kulala” Amesema Jaffo.
0 comments:
Post a Comment