Home » » “MWANAFUNZI SHULE YA MSINGI UHURU AKAMATWA ENEO LA BAR CHAKO NI CHAKO”

“MWANAFUNZI SHULE YA MSINGI UHURU AKAMATWA ENEO LA BAR CHAKO NI CHAKO”

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Judith Mhina-Maelezo

Ushirikiano wa Wazazi na Walimu –UWW wa Shule ya Msingi Uhuru Mkoa wa Dodoma, wamemkamata mwanafunzi akiwa katika eneo la Bar ya Chako ni Chako jana Jumanne tarehe 25 saa 3 asubuhi. Mwanafuzi huyo jina limehifadhiwa anasoma darasa la tatu ni mvulana ana umri wa miaka11 alikutwa hapo muda wa masomo .

Hayo yalisemwa na Mratibu wa Elimu wa Kata Uhuru Bibi Mary Rweikiza katika Manispaa ya Dodoma. Akisimulia mkasa huo Bi Mary alisema, mmoja wa wazazi wa Ushirikiano wa Wazazi na Walimu Bw Juma Hamisi alikuwa anapita katika eneo hilo na kumuona kijana huyo akiwa anacheza hapo Bar na Watoto wanaishi katika mazingira magumu.

Aidha, Mratibu Bibi Rweikiza ambaye ni mmoja wa washiriki wa semina ya Mawasiliano ya Mpango wa Kuboresha na Kuinua Kiwango cha Ubora wa Elimu Tanzania EQUIP- Tanzania, ndio chanzo cha uundwaji wa Ushirikiano wa Wazazi na Waalimu katika Mkoa mzima wa Dodoma.

Bibi Oliver Kapaya Mratibu wa Semina ya Mawasiliano ya Mpango wa Kuboresha na Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania alisema Ushirikiano huu wa Wazazi na Waalimu unaundwa baada ya kuitisha kikao cha wazazi wa shule husika, wanachagua wazazi 2 wawakilishi kila darasa kwa kuzingatia jinsia na mwalimu mmoja kila darasa,.


Baada kuwapata wawakilishi hao wanachagua Mratibu wa umoja huo, kwa ujumla ushirikiano huu unakuwa na wawakilishi 21., wazazi 14 kwa jinsia sawa na walimu 7.

Majukumu ya Ushirikiano huo ni kusaidia kuimarisha ustawi wa wanafunzi shuleni, kudhibiti utoro, kutoa taarifa au habari mbalimbali za shule kwa jamii husika na Taifa kwa ujumla. Aidha, malengo ni kutatua migogoro baina ya shule yenyewe na jamii,  kutoa ushauri na unasihi, kuthibiti nidhamu, na kurejesha umakini kwa wanafuzi katika kupata elimu,  kuweza kubaini aina za unyanyasaji shuleni na kutafuta ufumbuzi wake. Na mwisho kusimamia shughuli za Klabu za wanafunzi, michezo, ubunifu. Makambi ya masomo

Bibi Kapaya aliongeza kwa kusema matokeo, ya Ushikiano huu umefanya wazazi kuelewa majukumu yao kwa watoto, pia wazazi kuwa sehemu ya shule na katika kufanya maamuzi, kuboresha mahusiano kati ya shule na jamii, kuboresha mahusiano kati ya shule na jamii, kuinua kiwango cha ubora na ufaulu katika shule, kuboresha hali ya ustawi wa wananfunzi ikiwa kuboresha afya zao na matumizi sahihi ya mazingira yanayowazunguka.

Mkoa wa Dodoma una jumla ya shule za Msingi 727 ambapo kila shule ina wanafuzi kati ya idadi ya juu 1,500 na ya chini 250 na shule zote hizo zina utendaji wa Ushirikiano wa Wazazi na Walimu – UWW.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa