MCHENGERWA: SERIKALI IMEDHAMIRIA KUBORESHA MAISHA YA WALIMU NCHINI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema Serikali sikivu ya Awamu ya Sita imejidhatiti katika kuboresha maisha ya walimu nchini, hususani katika maeneo ya maslahi na mazingira ya kazi.

Mhe. Mchengerwa amesema hayo wakati akizungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Wilaya ya Rufiji, mara baada ya walimu hao kufanya uchaguzi wa viongozi uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Maendeleo Ikwiriri.

“Tumedhamiria kuboresha maisha yenu. Binafsi, tangu nikiwa Waziri wa UTUMISHI hadi sasa nikiwa Waziri wa TAMISEMI, nimekuwa mstari wa mbele kupigiania madaraja yenu na maslahi ya walimu kwa ujumla amesisitiza.

Aidha, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa Taifa lina bahati ya kuwa na Rais anayewajali na kuwathamini walimu na kwani baada ya kupokea ombi la kuwapandisha madaraja walimu, Rais hakusita kulitekeleza, licha ya ukweli kuwa hatua hiyo ilisababisha ongezeko katika bajeti ya mishahara.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Pwani, Bi. Susan Shesha, amemshukuru Waziri Mchengerwa kwa juhudi zake za kupigania maslahi ya walimu tangu akiwa Waziri wa UTUMISHI, na kueleza kuwa katika nafasi yake ya sasa kama Waziri wa TAMISEMI, ameendelea kutoa kipaumbele kwa walimu kwa kusimamia miradi ya elimu kwa uadilifu, ili kuhakikisha kuwa inawanufaisha wananchi kwa ujumla.



DENMARK KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA

Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma

Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu – El Maamry Mwamba, amefanya mazungumzo na ujumbe kutoka Danish Public Investment Fund for Development Countries (IFU), ukiongozwa na Balozi wa Denmark Nchini, Mhe. Jepser Kammersgaar, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dodoma.

Mazungumzo yao yalilenga kujadili fursa mbalimbali zikiwepo za mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za maji na nishati. 

Aidha, kupitia Mfuko huo Tanzania inaweza kunufaika na aina mbalimbali za ufadhili unaotolewa na Mfuko huo ikiwemo uwekezaji wa hisa (equity investment), na dhamana (guarantees).

Kikao hicho kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa IFU, anayeshughulikia Sekta ya Umma katika Mikopo Nafuu na Misaada, Bi. Tina Kollerup Hansen, na Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Dhamana, Bw. Theo Ib Larsen.

Kwa upande wa Wizara ya Fedha kikao hicho kilihudhuriwa na Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje, Bw. Melckzedeck Mbise na Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Bi. Tiba Kisonga.




RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA


Na WMJJWM- Dodoma 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewafuturisha Watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kikombo Dodoma katika Kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Akizungumza wakati wa Iftari hiyo iliyofanyka Machi 25,2025 kwa niaba yake, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis alitoa shukurani kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi yenye lengo la kuondoa kabisa changamoto zinazowakabili watoto walio katika mazingira hatarishi. 

“Kipekee kabisa, ninamshukuru tena Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kufuturisha watoto wanaoishi katika Makao ya Taifa ya Watoto Kikombo pamoja na maeneo mengine ya nchi hususani Watoto wa Mkoa wa Arusha na Dar Es Salaam”. ameeleza Naibu Waziri Mwanaidi.

Aidha aliongeza kuwa Wizara inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na wadau kwa lengo la kuhakikisha watoto walio katika mazingira hatarishi wanapatiwa huduma ya malezi ya muda mfupi katika Makao ya Watoto.

“Serikali na Wadau tutaendelea kushirikiana kutoa huduma kulingana na sheria, kanuni na miongozo tuliyojiwekea, nitumie fursa hii kuwaomba wamiliki wa makao ya kulelea watoto kuhakikisha mnatoa huduma kwa mtoto kwa kuzingatia maslahi mapana ya mtoto”. amesema Naibu Waziri Mwanaidi.

Mhe. Mwanaidi alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi, walezi na watendaji wa Wizara kwa kuendelea kuratibu na kusimamia utekelezaji wa afua za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto katika makao yote hapa nchini. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt.John Jingu amewasihi watoto waishio katika makao hayo kuishi kwa upendo na amani huku wakiweka bidii katika masomo yao na stadi za kazi kwa ujumla ili waweze kufikia malengo yao ya baadae.

Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Abbot fund Edna Hauli ameipongeza Serikali kwa juhudi zake katika kuhakiksha watoto wanakuwa salama na kuahidi kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yao muhimu na kuweza kufikia utimilifu wao kama binadamu.

Sanjari na hilo katika tukio hilo pia kuliambatana na tukio la kukabidhi mashine ya kufulia 4, printer na photocopy mashine 1, vitabu 1670 friji 2 nguo na mahitaji mengine ambavyo vilitolewa na Shirika la Abbot Fund vikiwa na thamani ya shiling Milioni 88 ili viweze kurahisisha majukumu ya utendaji kazi ndani ya Makao hayo.





COSTECH WAKABIDHI RASMI ENEO LA MRADI KWA MKANDARASI KWA AJILI YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA STI JIJINI DODOMA

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imekabidhi rasmi

 eneo la mradi kwa mkandarasi TIL Construction Limited kwa ajili 

ya kuanza ujenzi wa jengo jipya la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu

 (STI)  jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kukabidhi eneo hilo la mradi 

Machi 25,2025 jijini Dodoma  Mratibu Msaidizi wa Mradi

 wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) 

kutoka COSTECH, Dkt. Aloyce Andrew, amesema hatua hiyo

 inalenga kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau wa taasisi hiyo.

WMA YAELEZA MAFANIKIO YAKE IKIWEMO KUAJIRI WAFANYAKAZI 186




Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban 
Kihulla, amesema kuwa moja ya mafanikio makubwa
 na ya kihistoria ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan
 katika kipindi cha miaka minne ya utawala wake ni 
\kuajiri wafanyakazi 186, jambo ambalo limeleta
 mabadiliko makubwa katika ufanisi wa taasisi hiyo.

Kihulla ameeleza haya wakati akitoa ripoti ya mafanikio ya 
Serikali katika kipindi cha miaka minne ya utawala wa 
Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Ukumbi wa Idara ya 
Habari-MAELEZO, Jijini Dodoma.
Amesema kuwa,

NSSF YATOA ELIMU YA SKIMU YA TAIFA YA HIFADHI YA JAMII YA SEKTA ISIYO RASMI ILIYOBORESHWA KWA KAMATI YA BUNGE


Na MWANDISHI WETU,
DODOMA. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Skimu ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kwa Sekta isiyo Rasmi (National Informal Sector Scheme-NISS) iliyoboreshwa inalenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi waliojiajiri wenyewe kunufaika na mafao yanayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mhe. Ridhiwani alisema hayo mwanzoni mwa wiki hii wakati akifungua mafunzo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Ustawi na Maendeleo ya Jamii, iliyofanyika Bungeni Jijini Dodoma.

Amewahakikishia wajumbe wa kamati hiyo kuwa skimu hiyo imetengenezwa vizuri na ina faida kubwa kwa jamii kwani inatoa kinga dhidi ya majanga kama uzee, ulemavu, ugonjwa hivyo amewataka wabunge kuwa mabalozi wazuri wa skimu hiyo.

“Waheshimiwa wabunge nyinyi ni wawakilishi wa wananchi mna wajibu wa kuwaeleza Watanzania kuhusu skimu hii pamoja na faida zake ili waweze kujiunga na kuchangia kwa maisha yao ya sasa na ya baadaye,” amesema Mhe. Ridhiwani.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba amesema skimu hiyo imeanzishwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi waliojiajiri wenyewe katika shughuli za kiuchumi na kuwa wanufaika ni pamoja na wakulima, wavuvi, wafugaji, wachimbaji wadogo wa madini, mama lishe, bodaboda na wajasiriamali wengine wote.

Bw. Mshomba amesema mwanachama anapaswa kuchangia kiasi kisichopungua shilingi 30,000 ambapo atanufaika na fao la matibabu yeye mwenyewe au shilingi 52,200 ambapo atanufaika na matibabu yeye na familia yake.  Amesema mwanachama anaweza kuchangia kidogo kidogo kwa siku, wiki au mwezi na kuwa anapaswa kutumia namba ya kumbukumbu ya malipo (control number) kuwasilisha michango.

Akizungumzia namna ya kuchangia katika skimu hiyo, Meneja Mifumo wa NSSF, Bw. Mihayo Mathayo amesema wamerahisisha uchangiaji kupitia akaunti ya benki au wakala kwa kutumia namba ya kumbukumbu ya malipo (control number), kupitia simu ya kiganjani (Mitandao yote) kwa kutumia namba ya kumbukumbu ya malipo (control number).

Awali, Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Fatma Toufiq ameipongeza NSSF kwa kuboresha skimu hiyo ambayo inaenda kuwa mkombozi wa wananchi waliojiajiri wenyewe kwa kunufaika na mafao mbalimbali yanayotolewa na Mfuko



MRITHI WA KINANA KUPATIKANA JANUARI HII

Na Dotto Kwilasa, JamhuriMedia, Dodoma

BAADA ya kimya cha muda mrefu kuhusu nani anachukua nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM) jibu limepatikana ambapo anatarajiwa kupatikana kati ya January 18 au 19 mwaka huu.

Hatua hii ni mara baada ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Abdulrahman Kinaana kutangaza kustaafu kwenye nafasi hiyo tangu Julai mwaka jana kwa madai ya kutaka kupumzika ambapo Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan aliliridhia ombi lake.

Akizungumza leo Januari 7,2025 Jijini Dodoma, Katibu wa NEC,Itikadi , Uenezi na Mafunzo wa Chama hicho Amos Makala ameeleza kuwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti huwa haigombewi wala kujazwa fomu bali hutokana na mapendekezo ya Mkutano Mkuu na halmashauri kuu ya CCM.

“Niwaombe wanachama watu kuachana na taharuki zinazoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mrithi wa Makumu Mwenyekiti wa chama Abdulahman Kinana, nafasi hii haigombewi ila inapendekezwa, ” ameeleza Makala.

Makala amewaambia waandishi wa habari kuwa kwa sasa hakuna mchakato wowote wa mrithi wa nafasi hiyo ambaye atapatikana baada ya mapendekezo ya jina katika kikao cha Kamati kuu na Halmashauri kuu Taifa.

MISA TAN YAFANYA ZIARA PSSSF NA KUJIONEA UFANISI WA MFUKO HUO


Na Mwandishi wetu - Dodoma

Uongozi wa Taasisi ya vyombo vya habari Kusini Mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA Tan ) imefanya ziara ya kujenga mahusiano kwenye Makao Makuu ya Mfuko wa Hifadhi ya jamii wa PSSSF Jijini Dodoma na kujionea ufanisi wa mfuko huo kwenye kuwahudumia watanzania.

Mwenyekiti wa MISA Tan. Bwana Edwin Soko alisema lengo kuu la ziara hiyo ni uongozi mpya wa MISA Tan kujitambulisha kwa PSSSF ili kuongeza mahusiano na mfuko huo pamoja na kuona utendaji wa mfuko huo Kwa kuwa waandishi wa habari Tanzania ni wanafaika wa mfuko huo na ni mabalozi wazuri wa shughuli za PSSSF. wakiwemo wanachama wa MISA Tan.

"Nimejifunza mengi Kwa kutembelea Idara mbalimbali ndani ya PSSSF kama vile idara ya kupokea simu Kwa wateja(Call Centre), Idara ya huduma Kwa wateja, Idara ya mafao Kwa wateja na Idara ya utunzaji wa taarifa za wanachama, huko kote nimeona  umahiri wa wafanyakazi wa PSSSF kwenye kutoa huduma Kwa watanzania", alisema Soko.

Pia Bwana Soko alimpongeza  Mkurugenzi wa PSSSF Bwana Abdul-Razak Badru Idara  nzima ya  Mahusiano na Elimu Kwa umma kwa kufanya kazi vizuri hususani kwenye kuwa kiungo muhimu katika kutoa  taarifa za huduma mbalimbali za  PSSSF kwa vyombo vya habari Nchini ili kuwapa nafasi watanzania kupima ufanisi wa Mfuko huo.

Naye Bibi Regina Kumba  Afisa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa PSSSF alieleza kuwa majukumu makubwa ya PSSSF ni kusajiri wanachama, kukusanya michango , kuwekeza na kutoa mafao Kwa wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF  kupitia mafao ya ya muda mrefu kama vile mafao ya uzeeni, mafao ya ulemavu, mafao ya kifo na  mafao ya wategemezi.

Pia Bibi Kumba alieleza pia mafao ya muda mfupi yakiwemo , mafao ya kukosa ajira, na mafao ya uzazi.

Bibi Kumba alieleza kuwa, PSSF inafanya kazi kwa katika Kanda mbalimbali Kwa kutumia mifumo ya kisasa ya utunzaji wa kumbukumbu za wanachama Kwa lengo la kuboresha mahusiano na wateja wote wa PSSSF.

Kwa pamoja uongozi wa MISA Tan na idara ya Mahusiano na Elimu kwa Umma zimekubaliana kuendelea kushirikiana kwenye kufanya kazi kwa pamoja ikiwemo kuhamasisha waandishi wa habari kujiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya PSSSF pamoja na kuwa mabalozi wa wazuri wa PSSSF ili kujenga Leo yetu na kesho yetu Kwa pamoja.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa