Home » » PAMELA MAASAY :SIOGOPI KUVULIWA WADHIFA HUU

PAMELA MAASAY :SIOGOPI KUVULIWA WADHIFA HUU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Siku chache baada ya wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba (Ukawa) kutoka bungeni, Pamela Maasay amesema hana hofu ya kufukuzwa ujumbe wa Bunge hilo kwa sababu ya kutetea kazi iliyompeleka bungeni.
Maasay alikuwa akizungumzia maoni ya baadhi ya wajumbe, yaliyotaka waondolewa kwenye Bunge hilo kutokana na hatua waliyochukua. “Kuna maombi yametolewa yakitaka wajumbe tulioteuliwa na Rais (wale 201) tuliotoka bungeni tuvuliwe ujumbe, kimsingi sina hofu ya kuondolewa ndani ya hilo Bunge kwa sababu nasimamia Rasimu ya Katiba ambayo niliteuliwa kuifanyi kazi,”alisema.
Alisema kushiriki mijadala isiyo zingatia msimamo wa wananchi, ni kushiriki kunyima haki Watanzania na kutokuitendea haki kampuni yake ambayo kutokuwapo kwake kazini, inapoteza fedha.
Maasay anayetoka kundi la wajumbe wateule 201, alisema kutokuwepo kazini, mwajiri wake kampuni ya CocaCola Kwanza, inapoteza Sh400 milioni. Alise sababu ya kuungana na waliosusia Bunge ni kwa kuwa amegundua hakuna nia wala dhamira ya dhati ya kufanya kilichowapeleka.
“Bunge limekuwa la majigambo na mashairi, kila anayesimama kuchangia mjadala hajadili rasimu bali yale anayojisikia kueleza, kana kwamba hakuna kanuni,” alisema.
Alisema baada ya mwenendo wa Bunge kwenda kinyume na matarajio, CCM walipaswa kuwa wa kwanza kusitisha mchakato wa Katiba. Alibainisha kuwa hakuunga mkono kutoka nje ya Bunge hilo kwa sababu waliyofanya hivyo ni Ukawa, angefanya hivyo kwa kundi lolote.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa