Home » » ZITTO AMTAKA WAZIRI NYALANDU KUJIUZULU AKISHINDWA KUTOA TANGAZO GAZETINI LEO JIONI

ZITTO AMTAKA WAZIRI NYALANDU KUJIUZULU AKISHINDWA KUTOA TANGAZO GAZETINI LEO JIONI


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ifikapo leo jioni awe ametoa tangazo katika gazeti la serikali ili kuruhusu tozo mpya za mahoteli kwenye hifadhi la sivyo ajiuzulu cheo chake.

Sehemu ya ripoti inayoonyesha serikali inavyopoteza fedha nyingi kwa kukosa malipo ya tozo.
Zitto ameyasema hayo leo wakati akichangia kwenye majadiliano ya hoja za kamati bungeni.
Zitto amesema kuwa serikali inapoteza shilingi bilioni 2 kila mwezi kwa kitendo cha Waziri wa Utalii kutotoa tangazo katika gazeti la Serikali ili kuruhusu tozo mpya za mahoteli katika Hifadhi.
Tangu mwaka 2011 mpaka 2014, Serikali imepoteza tshs 80 bilioni.

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa