Home » » Ni ahadi ya Rais wazee watapata Pensheni

Ni ahadi ya Rais wazee watapata Pensheni

Serikali imesema inajipanga kuandaa mchakato mzuri utakaotumika katika kutoa pensheni kwa wazee wote hapa nchini ili kuheshimu mchango wao katika kuitumikia jamii.

Serikali imeyasema hayo Bungeni Mjini Dodoma ambapo Naibu waziri wa Wizara ya Kazi, Vijana na Ajira Anthon Mavunde amesema ni dhamira ya serikali na ni ahadi ya Rais Dkt John Magufuli na pia ni ilani ya chama cha Mapinduzi kwamba pensheni itatolewa kwa wazee ili kuheshimu mchango wao.

Majibu ya Serikali yametokana na swali ambalo ameuliza Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche (CHADEMA) aliyetaka kujua ni kwanini serikali haiheshimu mchango wa wazee ambao wamelitumikia taifa hili kwa muda mrefu na hawapati chochote huku serikali ikiendelea kutoa ahadi zisizotekelezeka.

Aidha Naibu Waziri Anthon Mavunde amewahakikishia wazee kwamba ahadi ya Rais ipo pale pale ila wavute subra ili serikali ipate nafasi ya kujipanga vizuri ili kuweza kuhimili wazee wote bila ubaguzi wowote.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa