Home » » Rais Kikwete akagua Ukumbi wa Bunge Maalum la Katiba Dodoma

Rais Kikwete akagua Ukumbi wa Bunge Maalum la Katiba Dodoma

b6
Picha juu na chini ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua sehemu ya kukalia katika  Bunge jijini Dodoma alikotembea kukagua ukarabati na marekebisho yanayoendelea tayari kwa kupokea wajumbe wa Bunge la Katiba baadaye mwezi huu. Pichani juu kulia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Anne Makinda na kushoto ni WAZIRI wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi.
b5
b7
b4
b2
  Picha juu na chini ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembezwa sehemu mbalimbali za majengo ya Bunge jijini Dodoma alikotembea kukagua ukarabati na marekebisho  tayari kwa kupokea wajumbe wa Bunge la katiba baadaye mwezi huu.
b3
b1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi inayokarabati na kufanyia marekebisho ukumbi wa bunge mjini Dodoma tayari kwa kupokea wajumbe wa Bunge la katiba baadaye mwezi huu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Jumamosi, Februari Mosi, 2014, amekagua na kuridhishwa na kazi na kasi ya marekebisho yanayofanywa katika Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya Vikao vya Bunge Maalum la Katiba linaloanza baadaye mwezi huu.
Rais Kikwete amesimama kwa muda mjini Dodoma kujiridhisha na mwenendo wa maandalizi ya Bunge Maalum akiwa njiani kwenda Mbeya ambako atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili.
Rais Kikwete amekagua Ukumbi huo na huduma nyingine muhimu kwa ajili ya vikao hivyo ikiwa ni pamoja na bwalo la chakula kwa kiasi cha dakika 45 na kuvutiwa na mwenendo wa kazi na kasi ya marekebisho kwenye ukumbi huo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa William Lukuvi amemhakikishia Rais Kikwete kuwa kazi yote ya kufunga viti na vipaza sauti, ambavyo vitatumia mfumo wa kisasa wa mawasiliano ya kadi, ndani ya ukumbi huo itakuwa imekamilika ifikapo Februari 10, mwaka huu, siku tisa kuanzia sasa.
Baada ya kusikiliza maelezo hayo, Rais Kikwete amesema kuwa ni vizuri uongozi unaosimamia kazi hiyo ukajipa kiasi cha wiki moja baada ya Februari 10 kuhakikisha kuwa kweli kila mfuko unafanya kazi kabla ya shughuli za Bunge Maalum la Katiba kuanza rasmi kwa kufunguliwa na Mheshimiwa Rais mwenyewe.
Rais Kikwete amewaambia watumishi wa Serikali na Bunge waliomtembeza kwenye ukaguzi huo akiwamo Spika wa Bunge Mheshimiwa Anna Makinda na Katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashilila: “Nawapongeza sana kwa kuchapa kazi kwa kasi na ufanisi. Kazi hii imekwenda kwa haraka sana kwa kutilia maanani kilipomalizika kikao cha mwisho cha Bunge.”
Wakati Rais Kikwete akikagua huduma hizo, mafundi wa stadi mbali mbali walikuwa wanaendelea na kazi ikiwa ni pamoja na kufunga viti vyenye rangi nyekundu na Nembo ya Taifa kwenye ukumbi huo.
Bunge Maalum litakuwa na wajumbe 645 ambao ni Wabunge wa sasa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na Wajumbe 201 ambao watateuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya makundi mbali ambayo yanatajwa katika Sheria ya Marekebisho ya Katiba.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa