Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Miongoni mambo yaliyozungumzwa na
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na
kuibua hisia za wajumbe ni suala la uraia, maadili ya viongozi wa umma
pamoja na utaratibu wa kumpata Rais.
Suala la uraia pengine ndilo linaloweza kuelezwa
kwamba liliwakera baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ambao
hawakutaka uraia uwe wa Jamhuri ya Muungano, badala yake walikuwa
wakitaka uwe wa nchi washirika.
Kwa mujibu wa Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa
bungeni jana na Jaji Warioba, uraia utakuwa ni mmoja wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na umeorodheshwa miongoni mwa mambo ya Muungano.
“Uraia ni msingi wa utambulisho unaompa raia haki
ya kulindwa na nchi yake, ikiwa ni pamoja na haki zake za binadamu za
asili na zisizoondosheka kama zilivyotambuliwa au zitakavyotambuliwa,”
alisema na kufuatiwa na kelele za baadhi ya wajumbe zilizoashiria
kutokukubaliana naye.
Jaji Warioba hakujali kelele hizo na kuendelea:
“Uraia ndiyo kigezo na sifa ya kupewa dhamana ya uongozi wa taifa na
kuajiriwa katika mihimili ya Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama.
Rasimu inapendekeza kutambuliwa kwa uraia wa kuzaliwa na uraia wa
kujiandikisha ambao katika kujidhihirisha kwake, ni uraia wa nchi moja
usiojenga au kuleta hisia za kuwabagua au kuwatenga raia katika matabaka
na madaraja yanayotokana na tofauti ya hali au fursa zao.”
Kuhusu taasisi ya urais, Warioba alisema kuna
mapendekezo manne makubwa ambayo ni kumwondoa Rais kutoka kwenye Bunge,
namna atakavyochaguliwa, matokeo yake kuhojiwa mahakamani pamoja na
kupunguzwa kwa madaraka yake.
Jaji Warioba alisema wananchi pia walizungumzia
kuporomoka maadili ya viongozi na kuwa Sekretarieti ya Maadili ya
Viongozi iliyopo haina mamlaka ya kutosha ya kuchukua hatua.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment