Home » » JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA KUWASILISHA RASIMU YA KATIBA KESHO JUMANNE

JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA KUWASILISHA RASIMU YA KATIBA KESHO JUMANNE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akiwa na Makamu wake Jaji Augustino Ramadhani baada ya kuwasili bungeni mjini Dodoma na muda mfupi kabla ya kuanza  kuwasilisha rasimu ya Katiba Mpya. 
 Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba  wakiwa wamesimama kupinga Jaji Joseph Warioba asiwasilishe rasimu ya katiba huku wakipiga kelele na kugomga meza.
 Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba  wakiwa wamesimama kupinga Jaji Joseph Warioba asiwasilishe rasimu ya katiba 

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akijiandaa kuwasilisha rasimu ya Katiba Mpya. Hata hivyo zoezi hilo liliahirishwa hadi kesho wakati baadhi ya wajumbe waliposimama na kutaka  baadhi ya kanuni walizojiwekea zifuatwe, baada ya kuonekana hazikufuatwa. 
 Muafaka ulifikiwa baadaye na rasimu hiyo itawasilishwa kesho kwa Jaji Warioba kufanya hivyo kwa masaa manne badala ya moja ama mawili yaliyopendekezwa awali.  Habari kamili  zitawajia muda mfupi ujao...

Picha na Deusdedit Moshi 

wa Globu ya Jamii, Dodoma
Michuzi Media Group

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa