Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Nembo ya Dira ya Jukwaa la Katiba Tanzania.
Mwenyekiti
wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) Deus Kibamba (kulia), akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu mambo
muhimu ya kuzingatiwa baada ya makubaliano ya kuahirisha mchakato wa
Katiba Mpya baada ya Uchaguzi Mkuu 2015. Kushoto ni Mratibu wa Mtandao
wa Mapambano ya Ukimwi kwa Wanaume Tanzania (WOFATA), Alex Margery.
(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu 0712-727062)
Mwenyekiti
wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) Deus Kibamba (kulia), akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu mambo
muhimu ya kuzingatiwa baada ya makubaliano ya kuahirisha mchakato wa
Katiba Mpya baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti
wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) Deus Kibamba (wa pili kulia)
akizungumza katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Mratibu wa Jukata, Diana
Kidara, Mratibu wa
Mtandao wa Mapambano ya Ukimwi kwa Wanaume Tanzania (WOFATA), Alex
Margery na Mjumbe wa Bodi kutoka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye
ulemavu Tanzania (Shivyawata), Maria Chale.
Wapiga picha wa vyombo vya habari wakichukua tukio hilo.
Dotto Mwaibale
JUKWAA
la Katiba Tanzania (Jukata) limesema iwapo Bunge maalumu la Katiba
litaendelea mjini Dodoma baada ya mchakato wake kusitishwa kupisha
uchaguzi mkuu wa 2015 watakwenda kufunga kwa kufuri milango ya jengo
hilo ili kuokoa fedha za watanzania zinazotumika vibaya kwa kulipana
posho.
Katika
hatua nyingine Jukata limetangaza jimbo la uchaguzi la Samueli Sita
kuwa lipo wazi na nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Fredirick
Werema kuwa wazi baada ya kuwatuhumu kuchangia kwa kiasi kikubwa
kuharibu mchakato huo wa katiba mpya.
Hayo
yalibainishwa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus
Kibamba wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo
kuhusu mambo muhimu ya kuzingatiwa baada ya makubaliano ya kuahirisha
mchakato wa Katiba Mpya baada ya Uchaguzi Mkuu 2015
"Nafasi
za Sita na Werema tunatangaza kuwa sasa zipo wazi baada ya kupoteza
sifa za kuongoza kufuatia kuvuruga mchakato wa katiba mpya na kuwa
katika kipindi cha miaka 10 hawatakiwi kugombea nafasi yoyote katika
nchi hii hata iwe ya mjumbe wa shina" alisema Kibamba.
Kibamba
alivipongeza vyama vya siasa vilivyochini ya Kituo cha Demokrasia
Tanzania (TCD) kwa makubaliano yaliyofanyika na Rais Jakaya Kikwete
Agosti 8 mwaka huu Ikulu ndogo ya Chamwino Dodoma kuwa ni ya faraja na
matumaini makubwa kwa taifa.
Alisema
kutokana na mazungumzo hayo imekubalika kuwa mchakato wa Katiba mpya
uahirishwe kwa sasa hadi baada ya uchaguzi Mkuu wa 2015.
Akizungumzia
kuhusu kufunga milango ya jengo la Bunge ili asiingie mtu alisema hilo
litafanyika baada wiki mbili kuanzia leo iwapo tu wabunge hao
wataendelea na mchakato wa katiba hiyo na kuwa tukio hilo watalifanya
kwa umoja wao.
Kibamba
aliongeza kuwa kutokana na masuala ya Katiba kuwa na unyeti kwa taifa
zima na kwa jinsi yanavyoshikamana na masuala ya uchaguzi ambayo nayo
yana wadau wengi nje ya wanasiasa Jukata wanaona kuna haja ya kupanua
wigo wa mazungumzo na makubaliano yanayoendelea na yatakayokuja siku na
miezi ijayo yawe kwa taifa zima na si kwa wanasiasa.
"Jukata
pia tunapongeza uamuzi wa wanasiasa kuahirisha uchaguzi wa serikali za
mitaa uliokuwa ufanyike mwezi Septemba 2014 mpaka mwaka 2015 hata hivyo
zipo hoja za msingi kuhusu uchaguzi huo" alisema Kibamba.
0 comments:
Post a Comment