Home » » Mzimu wa GPA waibuka bungeni

Mzimu wa GPA waibuka bungeni

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Profesa Joyce NdalichakoNa Elizabeth Hombo, Dodoma
SERIKALI imesema itaendelea kuvitambua vyeti vya wanafunzi waliomaliza na kupangiwa madaraja katika mfumo wa GPA licha ya kurudi katika mfumo wa divisheni kwa sasa.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ambaye alikiri kuwepo changamoto nyingi ambazo hutokea kulingana na mahitaji ya wakati husika na maoni ya wadau.
Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), Profesa Ndalichako alisema mpango wa Serikali ni kupokea maoni kutoka kwa wanajamii kulingana na mahitaji ya wakati huo na mfumo wa marekebisho nayo hufanywa kulingana na nyakati.
Katika swali lake la msingi, Waitara alitaka kujua lini Serikali itapeleka bungeni marekebisho ya sheria ya NECTA kwenye kifungu hicho ili kuondoa nguvu ya waziri kutoa maelekezo bila kuhoji wala kushirikisha wataalamu wa elimu.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Stella Manyanya, alisema kifungu hicho kinampa mamlaka waziri mwenye dhamana ya elimu kufanya maamuzi kwa niaba ya Serikali pale inapolazimu.
Alisema maamuzi hayo huzingatia wakati, mazingira halisi na matokeo ya tafiti mbalimbali kutoka kwa wataalamu pamoja na maoni ya wadau wa elimu ambapo Baraza la Mitihani hutakiwa kuyatekeleza.
“Serikali kwa sasa haina mpango wa kukifanyia marekebisho kifungu hicho cha Baraza kwa kuwa kinamwezesha waziri kutekeleza mahitaji ya wakati huo.
Chanzo Gazeti la Mtanzania
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa