Home » » WATU WANNE WAFARIKI BAADA YA BASI LA ABOOD KUGONGA TOYOTA IST BUNJU

WATU WANNE WAFARIKI BAADA YA BASI LA ABOOD KUGONGA TOYOTA IST BUNJU

Watu wanne wamefariki dunia baada ya basi la kampuni ya Abood kugongana na gari dogo aina ya Toyota IST katika eneo la Bunju Sokoni, Barabara ya Bagamoyo, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, ajali hiyo ilitokea Septemba 7, 2026, majira ya saa 1:40 usiku.

 Basi lenye namba za usajili T 235 EMJ, aina ya Yutong, liligongana na gari lenye namba T 274 ERU, aina ya Toyota IST.

 Basi hilo lilikuwa likitokea Tegeta kuelekea Bunju, likiwa na safari ya kwenda mkoani Tanga. Lilikuwa likiendeshwa na Christivian Steven Shemuhilu, mwenye umri wa miaka 38, mkazi wa Kange, Tanga.



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa