Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, ajali hiyo ilitokea Septemba 7, 2026, majira ya saa 1:40 usiku.
Basi lenye namba za usajili T 235 EMJ, aina ya Yutong, liligongana na gari lenye namba T 274 ERU, aina ya Toyota IST.
Basi hilo lilikuwa likitokea Tegeta kuelekea Bunju, likiwa na safari ya kwenda mkoani Tanga. Lilikuwa likiendeshwa na Christivian Steven Shemuhilu, mwenye umri wa miaka 38, mkazi wa Kange, Tanga.


0 comments:
Post a Comment