Home » » WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MAKAZI MAPYA YA WAZIRI MKUU NA UKARABATI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE MKOANI DODOMA

WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MAKAZI MAPYA YA WAZIRI MKUU NA UKARABATI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE MKOANI DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZIRI MHAGAMA: KAMILISHENI UKARABATI WA NYUMBA ZA WATUMISHI MWISHO WA MWEZI HUU.
Na Daudi Manongi-MANONGI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama amemwagiza mkandarasi anayesimamia ukarabati wa nyumba watakazo ishi watumishi wake kukabidhi nyumba hizo ifikapo tarehe 28 Mwezi huu.
Ameyasema hayo wakati akikagua ukarabati  wa makazi ya watumishi wake yaliyopo eneo la kikuyu mkoani Dodoma yanayosimamamiwa na Mamlaka ya Ustawishaji wa makao makuu Dodoma(CDA).
“Kama wote mnakumbuka agizo la mheshimiwa Waziri mkuu kwamba kufikia mwezi Februari mwakani Mawaziri wote,Manaibu Waziri,Makatibu wakuu na Manaibu wake pamoja na sehemu ya watumishi wachache wa kila wizara lazima wawe wameshafika Dodoma na leo tupo hapa kuhakikisha miundombinu iko sawa tayari kwa kazi ambayo tunataka kuifanya tukiwa hapa Dodoma,”Alisema Mhe.Mhagama
Aidha amesema kuwa nyumba hizo zimefikia katika hatua nzuri sana na hivyo ikifika februari wataanza kuhamia kama ilivyoagizwa.
Pia Waziri Mhagama amesema kuwa Ujenzi wa makazi ya Waziri Mkuu pia yamefikia hatua nzuri ambapo kwa sasa wanakamilisha uwekwaji wa tenki la maji ambalo litasaidia kuhifadhi lita laki mbili kwa siku kwa ajili ya matumizi  ya kila siku na pia ujenzi wa barabara mbili zinazofika Ofisi ya Waziri Mkuu mkandarasi ameshakamilisha ujenzi wa barabara hizo tayari kwa matumizi.
Mhe.Mhagama amewahakikishia watanzania na Serikali kwa Ujumla kuwa kufikia Mwezi Februari watahamia Dodoma ili kukamilisha agizo la rais wetu wa awamu ya tano na pia kukamilisha ndoto ya mwalimu Nyerere ya kuihamisha Serikali Dodoma.
MWISHO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa