Home » » PUMA, TIPER WATOA GAWIO BILIONI 9/-

PUMA, TIPER WATOA GAWIO BILIONI 9/-

Imeandikwa na Anastazia Anyimike, Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango.

 SERIKALI imepokea Sh bilioni tisa kama gawiwo kutoka kwenye kampuni mbili ambazo serikali ina hisa.
Aidha, serikali imekubali kulifanyia kazi ombi la Kampuni ya Mafuta ya Puma Energy la kutaka taasisi za umma, ziwe zinanunua mafuta ya kampuni hiyo yenye ubia wa asilimia 50 kwa 50 na serikali ili faida inayopatikana itumike kwenye kutatua changamoto za Watanzania.
Kampuni ya Mafuta ya Puma Renergy imetoa gawiwo la Sh bilioni saba wakati Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya Tanzania (TIPER) imetoa gawiwo la Sh bilioni mbili. Akijibu ombi lililotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Puma, Dk Ben Moshi, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango (pichani) wakati akipokea gawio la Sh bilioni saba kwa serikali ambayo ni faida iliyopatikana kutokana na biashara ya mafuta, alisema watalifanyia kazi hasa kwa kutambua mchango wa kampuni zilizowekeza nchini na zina ubia na serikali, na kutoa angalizo kuwa pamoja na ombi hilo kufanyiwa kazi, hakuna sababu ya Puma kubweteka kwani lazima ushindani uwepo ili kupatikana bidhaa bora.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa