Home » » JESHI LA POLISI DODOMA LAKAMATA MIRUNGI BUNDA 24

JESHI LA POLISI DODOMA LAKAMATA MIRUNGI BUNDA 24



Mnamo

tarehe 22/04/2012 majira ya saa 13:15 mchana katika eneo la Kibaigwa  
Wilaya ya Kongwa, Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata Mirungi bunda 
ishirini na nne (24), yenye thamani ya shillingi laki moja na kumi na 
saba elfu.

Katika tukio hilo watu wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani 
humo kwa tuhuma za kukutwa na mirungi hiyo, watuhumiwa hao ni  ABDUL S/O
AHMED FARAH, Maarufu kama CHIFU, mwenye umri wa miaka (40), na OMARY 
S/O HASH FARAH miaka (50) wote wakazi wa Kibaigwa.

Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa toka kwa wananchi kuwa kuna 
watu  wanafanya biashara ya kuuza Mirungi, ndipo Polisi waliweka mtego 
na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja Bw. OMARY S/O HASH FARAH akiwa 
na ruba moja (bunda moja) alilokuwa anataka kuliuza kwa  mtu aliyewekwa 
kama mtego.

Aidha Baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo, ndipo mtuhumiwa mwenzake 
akajifungia chumbani ili asikamatwe, lakini baada ya kukamatwa na 
alipopekuliwa akakutwa na ruba nyingine ishirini na tatu (23) ndani ya 
nyumba walimokuwa wakiishi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linapenda kutoa pongezi kwa wananchi, 
waliohusika kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu hao, ambao kwa 
kushirikiana na Jeshi la Polisi walifanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa 
hao. 

Mwisho napenda kutoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutekeleza dhana 
nzima ya Polisi Jamii na Ulinzi shirikishi, ili kuhakikisha maeneo yetu 
tunayoishi yanakuwa ya Utulivu, Amani na Salama na  hivyo kusaidia 
kukuza ustawi wa jamii yetu.

Wakati huo huo,  mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la JOHN S/O LUGANJE, 
mwenye umri wa miaka hamsini na nne(54) mgogo, na mkulima mkazi wa 
kijiji cha chunju wilaya ya Mpwapwa amekutwa amekufa porini baada ya 
kujinyonga kwa shati alilokuwa amelivaa.

Kwa mujibu wa Taarifa za Jeshi la Polisi Wilayani Mpwapwa, marehemu 
aligundulika amekufa porini majira ya saa nane mchana, siku ya jumamosi 
tarehe 21/04/2012, na kwamba alikuwa ametoweka nyumbani kwake toka 
tarehe 16/04/2012.

Hata hivyo taarifa toka kitongoji cha Ng’ongwa katika kijiji cha Chunyu 
zinasema marehemu alikuwa mgonjwa wa akili, hata hivyo Jeshi la polisi 
linaendelea na upelelezi wa tukio hilo.

Imetolewa na: SACP - Zelothe Steven 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa