Home » » DC Mpwapwa asitisha uchimbaji madini

DC Mpwapwa asitisha uchimbaji madini


Mwandishi Maalumu, Mpwapwa
MKUU  wa  Wilaya ya Mpwapwa,  Christopher Kangoye  amesitisha uchimbaji wa madini aina ya ‘copa’   katika Kata ya Lumuma  kwa kampuni ya  Kimani Minerals Limited kwa madai ya kutofuata taratibu na kuharibu mazingira 

Kangoye alisema alifikia hatua hiyo kutokana na mgogoro ulioibuka kati ya
mwekezaji huyo na  wanakijiji  wa kijiji hicho kwa madai kuwa mwekezaji huyo hajafuata  taratibu za uchimbaji wa madini.

Alisema wanakijiji hao wanadai kampuni hiyo inachimba madini kwenye vyanzo vya maji jambo linalohatarisha maisha ya wanakijiji hao.Mkuu wa wilaya alisema alisema  kampuni ina leseni ya wachimbaji Wadogo,  lakini wanatumia  mitambo ya kisasa katika kufanya utafiti wao ambao umejikita katika kuitafuta faida na kuwadhoofisha wachimbaji wadogo na wanakiji kwa ujumla.
Kangoye aliwataka watu wote wanaoishi kwenye vyanzo ya maji vya kijji hicho  kuondoka wenyewe kabla hajatumia  nguvu  za dola kwa ajili ya mstakabali wa Wilaya ya Mpwapwa na vitongoji vyake.

 “ Nasema hakuna aliye juu ya sheria,  hivyo wito wangu kwa wananchi na wawekezaji wafuate sheria na taratibu ili kuiendeleza Mpwapwa”, alisisitiza.

Alivitaja vijiji  ambavyo  wakazi wake wanaendesha shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji  kuwa ni Lufusi  katika Kata  ya Lumuma,  Kiboriani Mpwapwa mjini na Kwamdyanga  katika Kata ya Mpwapwa
mjini.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa  Shirika la Kuhifadhi Misitu ya
Asili ya  Tanzania,   Laurent Mwakakonyole  alidai  wawekezaji hao wameingia kwenye misitu ya asili.
Chanzo: Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa