Masoud Masasi,Dodoma yetu blogCHAMA cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Dodoma Mjini(DUFA)kimesemakinakabiliwa na ukata wa fedha za kuendeshea ligi ya wilayainayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa mwezi huu.Akizungumza na Mwananchi Katibu wa chama hicho Said Mohamedi alisemampaka sasa chama hicho kinahitaji sh 4,727,000 kwa ajili ya kuendeshealigi hiyo.Alisema fedha hizo zinatokana na gharama za kuwalipa waamuzi,posho zakamisaa na wasimamizi,huduma ya kwanza,matengenezo ya uwanja pamoja nazawadi za washindi.Mohamedi alisema wanategemea kupata sh 2,450,000 ambazo ni kwa ajiliya ada ya ushiriki wa ligi kwa timu 20 pamoja na viingilio vyauwanjani katika hatua ya sita bora jambo alilosema msaada unahitajikakwa wadau kuweza kukisaidia chama hicho.“Tunakabiliwa na ukata wa fedha za kuendeshea ligi yetu ya wilayaambayo inaanza mwezi huu tunawaomba wadau wa soka mkoani hapakujitokeza kusaidia soka la dodoma kwa misaada mbalimbali”alisemaBabuji.Katika hatua nyingine katibu huyo alisema jumla ya timu 22zimeshachukuwa fomu za ushiriki ambapo amesema mwisho wa kurudisha niSeptember 10 mwezi huu.
Home »
» CHAMA CHA SOKA DODOMA MJINI CHALIA NA PESA ZA KUENDESHEA LIGI YA WILAYA HIYO
0 comments:
Post a Comment