Home » » WAAMUZI WA SOKA DODOMA WATAKA FAINI WANAZOTOZWA TIMU KWA AJILI YA KUPIGA WAAMUZI NAO WAPEWE MGAO‏

WAAMUZI WA SOKA DODOMA WATAKA FAINI WANAZOTOZWA TIMU KWA AJILI YA KUPIGA WAAMUZI NAO WAPEWE MGAO‏


Masoud Masasi,Dodoma yetu Blog
WAAMUZI wa mchezo wa mpira wa miguu wamezitaka vyama vya mchezo huo
hapa nchini kuwepo kwa utaratibu wa kupatiwa mgao wa faini ambazo
wanazotozwa timu na wachezaji pindi mwamuzi anapojeruhiwa kwa kipigo.
Hatua hiyo inatokana na waamuzi hao kudai kuwa wanaposhambuliwa na
kujeruhiwa hakuna fungu lolote linalotoka kwa ajili ya matibabu zaidi
ya wao kujigharamia wenyewe huku faini hizo zikiingia ndani ya vyama
husika.
Wakizungumza wakati wa kikao kati ya waamuzi wa mkoa wa Dodoma na
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma(Dorefa)Nasoro
Kipenzi,waamuzi hao walisema kuwepo kwa utaratibu wa wao kugaiwa
kifuta jasho kutokana na faini hizo.
Mwamuzi Bam Bilasho alisema katika matukio hayo wakati mwingine
ujeruhiwa vibaya huku wakiibiwa vitu mbalimbali kutokana na
kushambuliwa lakini inapotokea timu kutozwa faini pesa zote uingia
ndani ya chama husika huku wao wakijigharamia kila kitu kutokana na
kupata majeraha.
Bilasho alisema kuwepo na utaratibu kwa kamati za nidhamu za vyama
mbalimbali hapa nchini kuweka utaratibu wa kuwapa mgao wa pesa
zinazotokana na faini ambazo upewa mwamuzi aliyejeruhiwa.
Mwamuzi mwingine Saleh Mang’ola alisema wao kama waamuzi huwa hawana
bima yoyote jambo alilosema wanapopata matatizo uishia kutoa fedha zao
mfukoni kujitibia jambo ambalo amesema wamekuwa wakibaguliwa sana.
Mang’ola aliongezea kuwa wamekuwa wakilipwa posho ndogo wanapokwenda
kuchezesha mechi mbalimbali na wakati mwingine huwa wanakopwa jambo
alilosema taaluma hiyo imekuwa haithaminiwi hapa nchini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Dorefa Nassoro Kipenzi aliwataka waamuzi
hao kuwa makini wakati wanapochezesha mechi zao ili kuepukana na fujo
zinazoweza kufanya kujeruhiwa huku akiwahidi kuboresha posho kwa
waamuzi wa mkoa huo kwenye mashindano yanayotambulika na chama hicho.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa