Home » » WAKULIMA WAMWANDIKIA BARUA PINDA

WAKULIMA WAMWANDIKIA BARUA PINDA



na Danson Kaijage, Kibaigwa
UMOJA wa wakulima wa Kibaigwa katika wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma na wakulima wa Kiteto mkoani Manyara wamelazimika kumwandikia barua Waziri Mkuu Mizengo Pinda kumwomba aingilie kati mgogoro kati yao na wafugaji katika wilaya hizo.
Wakulima hao wamechukua hatua hiyo ya kumwandikia barua Pinda kutokana na kulazimishwa na uongozi wa wilaya ya Kiteto wasiendelee kulima mahindi katika mashamba yao kwa madai kuwa ni maeneo ya wazi.
Barua hiyo iliyoandikwa Agosti 15, mwaka huu, inamwomba Waziri Mkuu aingilie kati mgogoro huo jambo linalosababisha uongozi wa mkoa wa Manyara kuwalazimisha wakulima kusitisha shughuli zao za kilimo cha kila siku.
Kwa mujibu ya barua hiyo, iwapo wakulima hawataruhusiwa kuendelea na kilimo katika mashamba yao, ni wazi kuwa watajikuta wakipelekwa jela kwa ajili ya kushindwa kurejesha mkopo wa trekta waliokopa hivi karibuni.
Hata hivyo walisema kuzuiliwa kuendelea na kilimo huku mashamba yao yakitumiwa na wafugaji kunaweza kuendeleza uhasama baina yao.
Mgogoro kati ya wakulima na wafugaji umedumu kwa miaka saba sasa na kufikia hatua ya watu kupoteza maisha kutokana na mapambano kati yao.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa