Masoud Masasi,DodomaWANANCHI wametakiwa kudumisha hifadhi ya misitu,uoto wa asili nauhifadhi wa mazingira ili kuweza kukabiliana na mabadiliko ya hali yahewa pamoja na tabia ya nchi.Pia wametakiwa kudumisha kilimo mseto na uchanganyaji bora wa mazaoya misitu,chakula na malisho ya mifugo kwa kutumia teknolojia rafikikwa mazingira ikiwa ni pamoja na miti yenye matumizi mazuri ya maji nainayoruhusuukuaji wa mazao ya miti yenyewe.Ushauri huo umetolewa na mhadhiri wa Chuo Kikuu chaDodoma(UDOM)upande wa hifadhi ya Bailojia na Mazingira Dr ChrispinusRubanza wakati alipokuwa akitoa mada mabadiliko ya hali ya hewa natabia ya nchi na athari zake kwa maendeleo ya nchi iliyofanyika katikatarafa ya Hombolo mkoani hapa.Rubanza alisema kuzuia uharibifu wa mazingira kwa kutochoma motomiti,kulima kilimo cha mseto na kuepukana na kilimo cha kuhama hamakutaweza kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.“Mabadiliko ya tabia ya nchi yanaweza kuepukika kwa kudumisha kilimocha mseto,kuzuia uharifu wa mazingira kwa kutochomo miti na kukata nakuepukana na kilimo cha kuhamahama kutosaidia kukabiliana na mabadilohaya”alisema Rubanza.Alisema athari za mabadiliko ya tabia ya nchi ni ukame unaotokana nauhaba wa maji,ongezeko la wadudu wa mazao na waletao magonjwa yamazao,mifugo na wanyamapori hapa nchini.Alibainisha kuwa hali itaweza kufanya kuwepo kwa upungufu wa akiba yachakula itakanayo na upunguaji wa uzalishaji wa mazao shambani.“Mabadiliko haya kwa kiwango kikubwa yanasababishwa na ongezeko lajoto duniani inafanya kubadilika kwa mikondo ya mvua,kubadilika kwakina cha bahari kubadilika kwa muelekeo wa kasi ya upepo na kuongezekakwa uwezekanowa kutokea kwa maafa kama vile ukame,mafuriko nakimbunga”alisema.
Home »
» WATANZANIA WATAKIWA KUEPUKNA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA ILI KUKABILIANA NA MABDILIKO YA TABIA NCHI
0 comments:
Post a Comment