Na Masoud Masasi- Dodoma yetu BlogWAZAZI na Walezi zaidi ya 20 wenye watoto wanaoishi na ulemavu wakutosikia wamesema mradi wa mafunzo ya lugha ya alama ya namba yakujifunza kwa mikono kwa herufi itakayowawezesha kupata mbinu namna yakuwasiliana kwa vitendo utaweza kuwasaidia wao kuweza kuwasiliana na watoto wao.Hayo yamebainishwa na Katibu wa Chama cha Chavita Wilaya ya KondoaAlly Jumanne alipokuwa akizungumza kwenye mafunzo ya lugha ya alamaya kujifunza kwa mikono herufi iliyowashirikisha wazazi na waleziwanaoishi na watoto wenye ulemavu wa kutosikia kutoka vijiji vya PahiWilaya ya Kondoa.Jumanne alisema kwenye Kata hiyo kuna idadi kubwa ya watoto wenyeulemavu wa kutosikia lakini changamoto iliyopo ni wazazi na walezi haokutofahamu jinsi ya mawasiliana kwa njia ya mikono kwa kutumiaalfabeti ambayo inayotumiwa na viziwi wote.“Kwenye kata hii kwa kweli kuna watoto wengi wenye ulemavu wakutosikia na changamoto iliyopo ni wazazi na walezi kutofahamu jinsiya kuweza kuwasiliana nao kwa kutumia mikono na alfabeti”alisemaJumanne.Alisema mafunzo yaliyoandaliwa kwa ufadhiri wa shirika lisilo laKiserila la The Foundation for Civic Society, waliyoyapata wazazi nawalezi yatawawezesha kutumia njia nyepesi ya kuwasiliana na watoto waowenye ulemavu huo tofauti na hapo awali ambapo walikuwa wakishindwakuelewana wao kwa wao katika mawasiliano .Hata hivyo alisema kuwa pamoja na mradi huyo wa mafunzo ya lugha yaalama Wilaya ya Kondoa bado viziwi wengi wanaoishi vijijiniwamebainika kutumia lugha ya asili badala ya lugha ya Taifainayokubalika na karibu mataifa mengi.Naye mwezeshaji wa mradi wa mafunzo wa lugha ya alama Wilaya ya KondoaMariam Athumani,aliiomba serikali mashirika na taasisi mbalimbalikukisaidia chama cha chavita Kondoa fedha ili kiweze kutoa elimu yalugha ya alama kwa watu wasioifahamu.Mariam alisema Chama hicho kikifadhiriwa kitaweza kuwafikia viziwiwalio wengi ambao wanaoishi vijijini ambao hawajui namna yakuwasiliana kwa kutumia lugha ya alama inayotumika ya Kitaifa.Kwa upande wake mratibu wa mradi wa mafunzo ya lugha ya alama Wilayaya Kondoa Mustapha Shabani amewataka wazazi na walezi kuungana nachama cha chavita kupinga usemi unaotumiwa wa kuwaita viziwi kwa jinala mabubu.Alisema viziwi wana mawasiliano yanayoweza kuwasiliana na mtu yoyotehivyo hakuna sababu ya kuwaita watu hao mabubu.
Home »
» WAZAZI WA WATOTO VIZIWI WAOMBA MAFUNZO YA LUGHA YA ALAMA
0 comments:
Post a Comment