Home » » DOREFA YABAINI TATIZO LA MIGOGORO YA SOKA DODOMA‏

DOREFA YABAINI TATIZO LA MIGOGORO YA SOKA DODOMA‏


Masoud Masasi,Dodoma yetu Blog
CHAMA cha mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma(Dorefa)kimesema kuwa kimebaini
moja ya migogoro inayojitokeza mkoani hapa inasababishwa na viongozi
na mashabiki wa soka kutokujua kabisa sheria za soka na kanuni za
mashindano hatua waliyosema ndio imekuwa chanzo cha migogoro
mbalimbali.
Hayo yalibainishwa na Mwenyekit wa Dorefa Nasoro kipenzi alipokuwa
akizungumza i juu ya migogoro mbalimbali ambayo imekuwa
ikijitokeza katika mashindano mbalimbali mkoani hapa.
Ibrahim alisema kuwa viongozi wengi wa vilabu vya soka pamoja na
mashabiki wamekuwa hawajui kwa kiasi kikubwa sheria za soka na kanuni
za mashindano jambo linalofanya kuwepo kwa migogoro ambayo haileti
tija kwa maendeleo ya soka la Dodoma.
“Baadhi ya viongozi wa vilabu na wapenzi kutokufahamu vyema sheria za
soka na kanuni za mashindano na hivyo kuwa ni chanzo cha migogoro
mbalimbali ambayo inatokana na wengi kutojua sheria na kanuni
hizo”alisema Ibrahim
Katibu huyo alisema chama hicho kimekuwa kikifanya semina elekezi
mbalimbali mkoani hapa kwa vilabu vyote vinavyoshiriki ligi mbalimbali
lengo likiwa ni kuhakikisha wanakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu
sheria na kanuni za mashindano ili kuepuka migogoro inayojitokeza.
"Tumekuwa tukifanya semina mbalimbali kwa vilabu vyetu vyote vya mkoa
wa Dodoma kila inapotokea mashindano mbalimbali na hii katika kusadia
kupunguza migogoro hiyo kwani tatizo ni kutojua sheria na kanuni za
mashindano na hii kidogo itasaidia"alisema katibu huyo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa