Dodoma. Viongozi wa dini wa madhehebu
mbalimbali mkoani Dodoma wamesema uharibifu wa mazingira nchini
unaongezeka kwa kasi hivyo ni wakati wa Serikali na taasisi za dini
kushirikiana kukabiliana na janga hilo.
Kwa misingi hiyo, wameitaka Serikali kupitia Ofisi
ya Makamu wa Rais (Mazingira), kuwashirikisha viongozi wa dini zote
nchini na kila mmoja atambue kuwa hilo ni tatizo linalohitaji mapambano
shirikishi.
Akizungumza katika kikao cha siku moja
kilichowajumuisha viongozi wa dini zote nchini, Askofu wa Kanisa la
Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Stephen Munga alisema Serikali
imewatenga viongozi wa dini wakati wao pia wana nafasi kubwa katika
jamii.
Alisema suala la kukabiliana na uharibifu huo ni pigo kwa watu wote hivyo ni vyema Serikali ikawashirikisha.
Chanzo;mwananchi
Chanzo;mwananchi
0 comments:
Post a Comment