Home » » BUNGE ;POSHO ZA MADEREVA WAJUMBE HAZITUHUSU

BUNGE ;POSHO ZA MADEREVA WAJUMBE HAZITUHUSU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Katibu wa Bunge,Dk. Thomas Kashililah.
 
Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, amesema suala la posho za madereva  halihusiani na taratibu wa uongozi wa bunge hilo.
 Kauli hiyo aliitoa jana alipokuwa  akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa bunge hilo halina uwezo wa kuajiri madereva.

Dk. Kashililah alisema utaratibu wa kuwalipa madereva upo chini ya wajumbe wenyewe ambao wamekwenda Dodoma na watumishi hao.

“Sisi tunalipa posho ya Sh 230,000 kwa mjumbe kama perdiem na Sh 70,000 ndiyo posho ya kikao husika, lakini katika hesabu hiyo, pesa za dereva ni Sh. 30,000 na 30,000 ni kwa ajili ya mafuta,” alisema Kashililah.

Alisema jambo linalowafanya wasiingilie malalamiko hayo ni kutokana na ukweli kuwa hawakuweka sheria rasmi kwa mjumbe kuwa na dereva.

Kuhusu wajumbe ambao hawana madereva, alisema ni haki yake kupewa kiasi hicho na kubaki nacho kwa kuwa anatumia njia zake za kumrahisishia kufanya shughuli zake za bunge.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa