Home » » KONDOMU MILIONI NANE ZAUZWA ARUSHA

KONDOMU MILIONI NANE ZAUZWA ARUSHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kondomu milioni nane zauzwa ArushaJUMLA ya pakiti milioni 8.2 za mipira ya kiume (kondomu), zimeuzwa
mkoani Arusha mwaka jana na idadi hiyo inatarajia kuongezeka mwaka huu hadi kufikia pakiti milioni 9.9.
Taarifa ya matumizi ya mipira hiyo ya kiume, imetolewa juzi jioni  mjini hapa na Geogre Magige, Meneja wa mikoa ya Arusha na
Manyara wa Shirika lisilo la kiserikali la Population Services International (PSI), ambalo hujishughulisha na uzalishaji na usambazaji wa kondomu nchini.
Magige alisema takwimu hizo zimetokana na utafiti wa mauzo ya bidhaa hizo kupitia
mawakala wao waliosambaa katika mkoa mzima wa Arusha kusaidia
kufikisha bidhaa hizo katika maeneo yote yenye mjumuiko wa watu
mbalimbali.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa