Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kuonyesha kutokukubaliana na uamuzi huo, Mchungaji Mtikila
alisimama bila kuruhusiwa na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pandu
Ameir Kificho na kuhoji sababu za kutopewa nafasi ya kuzungumza katika
Bunge hilo.
“Kwa nini unanizuia kuzungumza, unataka
nikuheshimu wakati heshima yangu unaivunja? Nataka kujua haki yangu,
nataka unijibu, nataka kujua kwanini hutaki nizungumze hapa ndani,”
alihoji.
Mtikila aliongeza kusema: “Unachagua watu wa
kuzungumza unachofurahia wewe ndicho kina haki ya kuzungumzwa hapa
ndani. Nataka kuzungumza ni haki yangu siyo kwa kupenda wewe ni haki
yangu. Unawapa watu ambao mnakubaliana na kupitisha kanuni mbovu na
wengine unatunyima kusema, siyo haki katika kutengeneza Katiba,”
alisema.
Kwa upande wake, Felix Mkosamali aliwasha kipaza
sauti na kusema hata yeye anashangaa hapewi nafasi ya kuzungumza
anapoomba kufanya hivyo. Alimtuhumu Mwenyekiti kwa kuwapa fursa hiyo
wajumbe ambao inaonekana walikubaliana naye kuunga mkono azimio.
Hata hivyo, Kificho aliwaomba radhi wajumbe ambao
hawakupata nafasi ya kuzungumza, akisema orodha ilikuwa ndefu na kwamba
isigewezekana kwa wote walioomba kupata fursa.
Wakati Mchungaji Mtikila na Mkosamali
wakizungumza, baadhi ya wajumbe waliendeleza utamaduni wa kuzomea licha
ya kwamba Kificho alishakemea hivi karibuni.
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi
wa Bunge, Mkosamali alisema siyo sahihi Bunge hilo kupitisha kanuni
ambazo hazina kifungu kinachoeleza namna ya kufanya uamuzi.
Mkosamali alisema kifungu cha 22(1) cha Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba kinamtaka mwenyekiti wa muda kusimamia uandaaji na
upitishwaji wa kanuni zote za Bunge Maalumu na siyo nusunusu.
Mbatia: Ilikuwa lazima tukubaliane
Mjumbe mwingine wa Bunge la Katiba, James Mbatia
alisema ilikuwa ni lazima wakubaliane na kupitisha Kanuni za Bunge hilo
ambazo katika mjadala wake, ziliwagawa wajumbe katika makundi mawili
yanayopingana.
Alipoulizwa sababu za kukubali kupita kwa kanuni
hizo wakati hazijakamilika, alisema: “Kila jambo linaundwa kwa
maridhiano na hata mwafaka wa Zanzibar ulipatikana baada ya pande mbili
zilizokuwa zikivutana kukubaliana.
Kwa upande wake, Profesa Ibrahim Lipumba alielezea
matumaini yake kuhusu kufikiwa mapema kwa maafikiano katika vifungu vya
37 na 38.
“Ninawapongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni na wewe (Kificho) kwa kutuletea kanuni zinazokidhi haja,” alisema.
Habari hii imeandaliwa na Kizitto Noya, Fidelis Butahe, Habel Chidawali, Daniel Mjema na Sharon Sauwa.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment