Home » » Makundi chanzo cha vurugu, mivutano Bunge la Katiba

Makundi chanzo cha vurugu, mivutano Bunge la Katiba

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mvutano unaoendelea ndani ya Bunge Maalum la Katiba unachangiwa kwa kiasi kikubwa na makundi yasiyo rasmi ya wanasiasa ambayo kwa bahati mbaya yanatambuliwa na Uongozi wa Bunge hilo.
Madai hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania, Peter Kuga Mziray, katika mkutano na wanahabari uliofanyika mjini Dodoma leo.
“Uwepo wa makundi haya na kutambuliwa kwake na bunge kunachochea mgawanyiko na kujenga uhasama baina ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,” alisema Mziray.
Hali hiyo imevuruga “dhana ya kufanya kazi pamoja” na kupelekea mashauriano yakwame, amesema Mziray, ambaye pia ni mjumbe wa Bunge la Katiba anayewakilisha Vyama vya Siasa.
Aliongeza: “[Majadiliano] yanakwama kwa sababu kamati ya uongozi kama imejaa wana CCM watupu, kila watakachokuja nacho pale kitakataliwa.”
Mwakilishi wa Vyama vya Wakulima Dk. Maselle Maziku anaamini tatizo haswa ni wanasiasa, na si vinginevyo.
“Vyama vya kisiasa vimekuwa vinafikia muafaka katika mambo mbalimbali na kutoa taswira kwamba kuna muelekeo mzuri, lakini baadae wanasiasa haohao wanabadilika na kuyabadili maridhiano hayo na kuanzisha mijadala mipya inayoturudisha nyuma.”
Maria Sarungi-Tsehai, anayewakilisha Mjumbe toka Taasisi Zisizokuwa Za Kiserikali anafikiri wajumbe wengi hawawathamini Wananchi waliowatuma Bungeni hapo, la sivyo wasingeendelea kuibua mijadala ambayo imeshasuluhishwa.
 “Tumepoteza hela za walipa kodi wiki 3 tunajadili kanuni tu, sasa kwa nini turudi wakati [tumeshapata] kamati, tunataka kuanza kazi, kwa nini tena suala la kanuni liibuliwe?” alihoji.
“Hapa watu hawana huruma na pesa za walipakodi.”
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa