Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Maji,Profesa Jumanne Maghembe amesema, masuala ya maji
na vyanzo vyake yatazungumziwa katika sheria na si katika Katiba
inayotakiwa kuandikwa kwa kifupi.
Profesa Maghembe aliyasema hayo jana mjini Dodoma
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Maji
inayofanyika mkoani Dodoma, kuanzia Jumatatu ijayo.
Profesa Maghembe alisema, Katiba ni sheria mama
inayotakiwa kubeba masuala ya msingi na kwa msingi huo mambo mengine
yataelekezwa katika sheria.
“Ukianza kuandika kila kitu katika Katiba
utajikuta unakuwa na kitabu kikubwa ambacho hata kubebeka
hakibebeki…masuala mengine yanatakiwa kuwekwa katika sheria ambayo ndiyo
inaweka utekelezaji wake,”alisema Profesa Maghembe.
Pia alisema katika kuhakikisha kuwa vyanzo vya
maji vinalindwa kikamilifu, wizara yake iko mbioni kukamilisha
mapendekezo ya marekebisho ya sheria itakayoongeza kiwango cha adhabu
kwa waharibifu .
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment