Home » » Nyang’anyi awashukia wenye uchu wa madaraka

Nyang’anyi awashukia wenye uchu wa madaraka

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Balozi Mustafa Nyang’anyi, amesema kushuka kwa uzalendo, uchu wa madaraka na chuki miongoni mwa Watanzania, ndiyo mambo yanayowasukuma baadhi ya watu kupiga kampeni ya kutaka muundo wa Serikali tatu.
Amesema hata hivyo, kampeni hizo ni sawa na kukashfu fikra za waasisi wa Taifa la Tanzania, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Hayati Mzee Abeid Aman Karume. Balozi Nyang’anyi, aliyasema hayo katikati ya wiki hii, alipokuwa akizungumza na gazeti hili kijijini kwake Kisese, wilayani Kondoa, Dodoma.
Alisema Muungano ni sawa na ndoa ambayo daima haiwezi kukosa changamoto na kwamba kwa msingi huo, watu badala ya kufikiria kuliongezea Taifa mzigo wa kugharimia Serikali tatu, ni vyema wakabaki na Serikali mbili.
Balozi Nyang’anyi alisema waasisi wa Muungano waliamua kwa makusudi kuwa na muundo wa Serikali mbili na kwamba walitanguliza mbele uzalendo kwa maslahi ya Tanzania.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa