Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Jakaya Kikwete amesema mambo ya Muungano yaliongezeka
kutoka 11 mpaka 22 kwa makubaliano kati ya pande zote mbili za Muungano.
Katika hotuba yake bungeni, Rais alisema siyo
kweli kwamba mambo hayo yaliongezwa kwa hila au kutokana na udhaifu wa
viongozi wa Zanzibar katika kutetea masilahi ya nchi hiyo.
Alisema kabla ya jambo lolote kuongezwa kwenye
Orodha ya Mambo ya Muungano, palifanyika makubaliano na mapendekezo
ambayo yalipelekwa bungeni na kujadiliwa.
Rais Kikwete alitoa historia ya namna mambo hayo
yalivyoongezwa kwenye Muungano na kutaja kuvunjika kwa iliyokuwa Jumuiya
ya Afrika Mashariki kuwa na moja ya sababu ya mambo ya Muungano
kuongezwa mara kwa mara.
Alisema mambo tisa kati ya 11 yaliyoongezeka yalitokana na kuvunjika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Kikwete alitaja sababu nyingine ya ongezeko
la mambo ya Muungano kuwa ni mabadiliko ya mfumo wa siasa, mwaka 1992
kutoka chama kimoja kwenda vyama vingi. “Ni mambo mawili tu yaliyotokana
na uamuzi na makubaliano ya nchi washirika wa Muungano,” alieleza.
Hata hivyo, alibainisha kuwapo kwa baadhi ya mambo
ambayo mbali na kutajwa kwenye Muungano, yanashughulikiwa na Zanzibar.
Aliyataja kuwa ni Bandari, Utafiti, Utabiri wa hali ya hewa, Leseni za
biashara na Takwimu na kwamba imethibitika inayamudu.
Rais Kikwete alibainisha kuwa walishakubaliana na
Rais Mstaafu Aman Abeid Karume na kwamba hata sasa wakati wa uongozi wa
Dk. Mohammed Ali Shein, makubaliano hayo bado yapo hai. Kilichokuwa
kikisubiriwa kuyatangaza, ni wakati mwafaka ambao alisema ni sasa.
Alishauri maboresho ya rasimu bungeni yazingatie
kuwa masuala ya uchumi na kuwa makini na athari za uamuzi wa kuchukua
muundo mpya wa Muungano.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment