Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAGONJWA 1,550 waliong’atwa na mbwa wanaozurura mitaani
wamepokelewa katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma mwaka jana ambapo kati
yao wanne walipoteza maisha.
Tangu kuanza kwa mwaka huu tayari watu sita wamepoteza maisha baada
ya kung’atwa na mbwa wazururaji bila kupata chanjo baada ya kujeruhiwa.
Akizungumza na Tanzania Daima katika mahojiano maalum
ofisini kwake, Mratibu wa huduma za chanjo na magonjwa yanayozuilika,
Paul Mageni, alisema kuna ongezeko la watu kung’atwa na mbwa wazururaji
Mkoa wa Dodoma.
Alisema katika hospitali hiyo wanapokea wagonjwa zaidi ya 10 kila
siku huku akibainisha kwamba waliofariki walichelewa kupata chanjo ama
hawakupata kabisa.
Kwa mujibu wa Mageni serikali ilikuwa ikitoa chanjo bure mara kwa
mara lakini hivi sasa utaratibu huo hakuna kwa kuwa serikali imesitisha
utoaji wa dawa za bure.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment